Sunday, November 1, 2015

NENE TCHAKOU MUUNGURUMISHA WA SOLO



NENE TCHAKOU MUUNGURUMISHA WA SOLO

Nene Tchakou ni jina ambalo halijazoweleka sana kwa wapenzi wengi wa muziki wa dansi. Ni mkung’utaji wa gitaa la solo aliyepitia katika bendi nyingi huko jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Jina lake halisi ni Nene Mbedi, kwa sasa ni mtu mzima wa umri wa miaka 57 hivi sasa. 

Alizaliwa Februari 1957, katika eneo lililojulikana kama Banana huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Vipaji vingi vya wanamuziki huibukia wakati wakiwa  Kanisani  wakiimba au kupiga ala ya muziki na wengine hutokea kwenye Madrasa wakiimba Kaswida. Lakini kwa Nene Tchakou kwake ilikuwa tofauti kabisa.

Mbendi Tchakou  alianza kujihusisha na maswala ya muziki akicharaza gita kwenye kundi lililokuwa linaundwa na watoto wa Askari jijini Kinshasa.

Nuru njema ya mafanikio katika muziki ilianza kung’aa mwaka 1973 akiwa na bendi ya Bella Negrita. Mafanikio hayo yalipelekea kuanza safari ndefu ya kuzunguka kwenye bendi kadha wa kadha.

Weledi wake katika muziki alifanywa mithiri ya kito cha thamani kwa kuwa kila alikotuwa, alikubalika vilivyo.

Safari yake ya mwaka ya 1981, ilimfikisha katika kundi lililokuwa maarufu la ‘Langa Langa Stars mahali alikopewa jina la ‘Tchakou,’ likiwa na maana ya Parrot kwa lugha ya Kilingala. Kwa Kiswahili ni ndege ajulikanaye kama Kasuku.

Tchakou hakuwa mtu wa kukata tamaa wakati akitafuta mfanikio zaidi. Aliendeza safari  mwaka 1983 alipojiunga katika bendi ya Grand Zaiko, ikiwa chini ya uongozi wa Pepe Manwaku.

Alitoa mchango mkubwa mno katika bendi hiyo hususani katika e kibao cha ‘Mbongo’. Baadaye akaamua kupiga muziki akijitegemea na kufanikiwa kufyatua wimbo wa ‘Niger’ mwaka 1987.

Ni kawaida kwa wanamuziki toka nchi za Afrika ya Kati pindi wanapokaribia mafanikio, hukimbilia kwenda nje ya nchi yao. Nene naye alifanya kwenda katika jiji Paris nchini Ufaransa mwaka 1988.

Alipokuwa katika jiji hilo aliandika historia kwa kutoa mchango mkubwa kwa nguli wa muziki barani Afrika, Kofi Olomide na kutoa albamu ya ‘Papa Bonheur’.

Alipenda sana kushiriki na wanamuziki wakubwa hivyo baada ya muda alijiunga na kundi la Soukous Stars linaloongozwa na Lokassa ya Mbongo. 

Hapo walianza matayarisho ya albamu iliyokuja kutamba vilivyo ya ‘Lagos Knight’.

Utaratibu wa kushirikiana na wanamuziki wakubwa aliuendeleza ambapo kwa mara nyingine alishirikiana na mwanamuziki Lala Nomotoki (kutoka Togo) Shi Loving (Kutoka Nigeria), Papa Wemba (Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, walitoa albamu ya ‘For idole.’

Ili atengeneze muziki mzuri Nene akashirikiana na mwimbaji mahiri Aurlus Mabele kutoka Congo Brazzavile, kwa pamoja wakaandaa albamu ya ‘Dossirr X’.

Nene Tchakou alitengeneza albamu yake ya kwanza akiwashirikisha Madame (Bongo), Patience Dabani (Kutoka Gabon), 3615 Code Niawu (Kutoka DRC.

Mwaka mmoja baadaye akiwa katika Jiji la California nchini Marekani, alirekodi albamu moja iliyotoka mwaka 2001.

Alimshirikisha mwimbaji wa Soukous Stars Shimmita mapema mwaka 2002, kuanzisha kundi la Afro Muzika.

Mwaka 2003 Nene Tchakou alijiunga na Lembo ya ‘Rowa Records’ kama msanii mkaazi. Huko ndiko alikotengeneza na kufyatua CD ya ‘Cesse Le Fou’ Pendin.

Tchakou vilevile anajishirikisha na kupiga muziki wa kiasili akishirikiana na wanamuziki wengine wa Kiafrika chini ya uongozi wa Injinia na Produza Rick Scott.

Nene Tchakou ameongeza idadi ya wanamuziki kwa Kiafrika wanaoishi nchini Marekani, na kwa idadi yao hadi sasa wamepatikana wanamuziki watatu.

Wanamuziki hao ni pamoja na Sam Mangwana, Diblo Dibala na  yeye Nene Tchakou.

Amesema bado wanahitaji wanamuziki wengi ili waendelee kuutangaza muziki wa Kiafrika Ulimwenguni kote.

Mwisho.





JOSEPH KABASELE ALIYETAMBA KWENYE MUZIKI WA DANSI



JOSEPH  KABASELE ALIYETAMBA KWENYE MUZIKI WA DANSI
                      

MUZIKI WA DANSI UNA HISTORIA NDEFU PIA UNA WAPENZI WENGI HAPA TANZANIA NA AFRIKA KWA UJUMLA.

PASIPO KUWATAJA BAADHI YA MAGWIJI UTAKUWA HUJAKAMILISHA HISTORIA NA MAELEZO YA MUZIKI UPASWAVYO KUSIMULIA.

JOSEPH KABASELA TSHAMA ‘GRAND KALLE’ NI MIONGONI MWA HAO ALIYEKUWA GWIJI WA MUZIKI HUO HAPA AFRIKA. 

HUYO NDIYE ALIYESAIDIA MUELEKEO WA MUZIKI WA KISASA HUKO JAMHURI YA KIDEMOKRASIA YA KONGO.

KABASELE 'GRAND KALLE' NDIYE ALIYEKUWA MUANZILISHI NA KIONGOZI WA BENDI YA AFRICAN JAZZ.

BENDI HIYO ILITOA WANAMUZIKI MAHIRI AKIWAMO MPIGA GITAA MAHIRI, DK. NICO KASANDA. AIDHA ILISHEHENI NGULI WENGINE AKINA TABU LEY ALIYEKUWA MTYUNZI NAMWIMBAJI WA BENDI HIYO. MPULIZAJI WA SAXOPHONE ‘MDOMO WA BATA’ MAARUFU MANU DIBANGO.

JOSEPH KABASELE ALIKUWA AKIITWA BABA WA MTINDO WA RUMBA PIA KINARA WA MUZIKI WA KIAFRIKA NA MIONGONI MWA WAIMBAJI NA WATUNZI WAKUBWA KATIKA BARA HILI LA AFRIKA YA WATU WEUSI WANAOZUNGUMZA KIFARANSA.


ALIZALIWA  KONGO - MATADI   KATIKA FAMILIA MAARUFU ILIYOMJUMUISHA JOSEPH MALULA AMBAYE ALITOKEA KUWA ASKOFU WA KANISA KATOLIKI. 

KABASELE ALIONDOKEA KUWA MIONGONI MWA WATU WA ZAMA HIZO WALIOELIMIKA. ALIMALIZA ELIMU YA SEKONDARI NA AKAAJIRIWA KAZI YA MPIGA MASHINE (TYPIST) KWENYE KAMPUNI ZA BIASHARA KATIKA JIJI LA LEOPOLDVILLE (KINSHASA).

MUZIKI ULIKUWA KAMA WITO WAKE NA AKAGUNDUA MWANYA WA KUUFUATILIA NA KWENYE MWAKA 1950 AKAWEPO KATIKA STUDIO MPYA ILIYOJULIKANA KWA JINA LA OPIKA.


KATIKA STUDIO HIYO, ALIUNGANA NA  WANAMUZIKI WA MUDA AMBAO WALIYEJULIKANA KWA JINA LA JIMMY ‘ZACHARIE ELENGA’ AMBAYE ALIKUWA NDIYE NYOTA WA WAKATI HUO. 

PIA WALIKUWEPO WAPIGA MAGITA MASHUHURI GEORGES DOULA NA ALBERT YAMBA YAMBA. BENDI HIYO HAIKUBAGUA WAPIGAJI WACHANGA AMBAO KAMA ALIVYOKUWA KWAKE YEYE, MWENYEWE WALIONA MUZIKI NDIO UFUNGUO WA MAFANIKIO BAADAYE WAKIWA NJE YA MIHANGAIKO YA KAZI NA PIA BAADA YA MAONEVU YA UKOLONI.


MSETO WA HUO KABASELE, DOULA NA YAMBA YAMBA, ULIIGWA NA BENDI NYINGINE  ILIYOJULIKANA KWA JINA LA OTC BAADA YA KUFANYA ‘PROMOSHENI’ YA FILAMU KWA AJILI YA RADIO STESHENI YA HAPO KINSHASA AMBAYO ILIKUWA IKITUMIA HERUFI HIZO – OTC.


KABASELE ALIWEZA KUBUNI MTINDO WAKE BAADA YA KUHAMASIKA NA KUMUONA MUIMBAJI MACHACHARI ‘TINO ROSI’ AMBAYE SAUTI YAKE YA KUGHANI NA YENYE MVUTO KWENYE NYIMBO ZAKE, ILIKUWA KIVUTIO KIKUBWA KWA WAKAZI WA MJI WA KINSHASA.

‘GRAND KALLE’ NYIMBO ZAKE ZA MWANZONI ZILIZO ZILIKUWA MITHIRI YA MOTO MKALI  WA KUOTE MBALI. ILIKUWA KAZI MARIDADI ILIYOTOKANA NA MJUMUIKO WA WANAMUZIKI VIJANA WA OPIKA, HUSUSANI MPIGA GITAA DK. NICO KASANDA NA MCHEZA GITAA LA KATI (RHYTHM), KAKA YAKE NICO, CHARLES ‘DECHAUD’ MWAMBA.

WIMBO PARAFIFI ULIOFYATULIWA MWAKA 1952, ULIKUWA NA  MAUDHUI YAKE YA KUMSIFIA MTANGAZAJI WA RADIO ALIYEKUWA KONGO  BRAZZAVILLE.

UTUNZI WA KABASELE ULIOWEZA KUTIA FORA  PAMOJA NA ULE ‘KALE KATO’ WA MWAKA 1952, ULIHADITHIA JUU YA PENZI LA KABASELE KWA KIMWANA MMOJA ALIYEJULIKANA KWA JINA LA ‘KATHERINE’.

WIMBO HUO ULIKUWA WA KWANZA WA KIKONGO KUCHEZWA KWA ALA YA ‘SAXOPHONE’, IKIMTUMIA MPULIAJI WA KUAZIMA ‘FUD CANDRIX’.


KATIKA KIPINDI CHA KWENYE MIAKA YA 1953 HADI 1955 BENDI MPYA ILIYOWAJUMUISHA JOSEPH KABASELE, DK. NICO KASANDA NA DECHAUD ILIIBUKA KUTOKA KUWA WANAMUZIKI WA MUDA WA STUDIO YA OPIKA WAKAJIITA AFRICAN JAZZ, WAKIAZIMA JINA HILO AMBALO HALIKUSHABIHIYANA NA MTINDO WA MUZIKI WA KIMAREKANI WA ‘JAZZ’ KAMA JINA LILIVYO.

AFRICAN JAZZ ILIPIGA MUZIKI WA NYIMBO ZAKILATINI NA BENDI ILICHANGIA KWA KIASI KIKUBWA KUKUA KWA RUMBA LA KIKONGO LILILOIBUKA KIPINDI HICHO.


KABASELE AKAJULIKANA KAMA ILIYEJULIKANA KAMA ‘LE GRAND KALLE’, UMAARUFU WAKE UKAWA HAUNA MFANO.

WAIMBAJI WENGINE KADHAA WALIANZA KUMUIGA STAILI ZAKE KIASI KWAMBA WATU WAKAANZA KUZUNGUMZIA KUANZISHWA KWA SHULE (MCHAPUO) WA KABASELE AU WA AFRICAN JAZZ.

AIDHA BAADHI YA NYOTA WENGINE ALIOKUWA NAO KATIKA AFRICAN JAZZ WALIKUWEPO WAIMBAJI JOSEPH MULAMBA MUJOS, BOMBENGA NA MPIGA GITA TINO BAROZA AMBAPO BENDI HIYO YA AFRICAN JAZZ ILIWEZA KUWEKA FURSA NZURI KUWA NI UWANJA WA MAFUNZO KWA WANAMUZIKI VIJANA WA KIZAZI KILICHOFUATIA KONGO.

HADI KUFIKIA MWAKA 1960 AFRICAN JAZZ ILIKUWA BENDI YA JUU NCHINI HUMO NA KUWEZA KUFYATUA MAELFU KADHAA YA SANTURI ZILIZOTOLEWA KATIKA NEMBO YA ‘DECCA’ NA KUWEZA KUWAPATA MASHABIKI WENGI KATIKA KUMBI MBALI MBALI.


JOSEPH KABASELE ALIKUWA KARIBU SANA NA KUNDI LA ROCK MAMBO, HIYO ILILETA MUUNGANO MZURI NA KUNDI LAKE LA AFRICAN JAZZ.

ALISHIRIKIANA NAO NA KUWEZA KUTOA VIBAO VYENYE VIWANGO VIZURI HASA ALIPOKUWA AMESHIRIKIANA NA JEAN SERGE ESSOUS, NINO MALAPET, ROSSIGNOL NA PANDI.


ILIPOTIMU MWEZI JANUARI 1960, KABASELE NA KUNDI LAKE LA AFRICAN JAZZ PAMOJA NA WAJUMBE WAWAKILISHI WA ILIYOKUWA ‘BELGIAN CONGO’ WALIFANYA KITU CHA KIHISTORIA AMBACHO NI KONGOMANO LA UTAMBULISHO  LA KISISASA HUKO BRUSSELS.

MIONGONI MWA TUNGO ZAKE ALIZOZIFANYA KATIKA KONGOMANO HILO LA KISIASA LA MWAKA HUO, NI UTUNZI WAKE ULIOJULIKANA KAMA ‘INDEPENDENCE CHA CHA’ NA ULE WA ‘LE TABLE RONDE’ AMBAO KWA PAMOJA ULITAMBULIKA KAMA WIMBO WA KITAIFA KUFIKIA UHURU.


UTUNZI MWINGINE WA KABASELE ‘BILOMBE BA GAGNE’ (WENYE MAANA WENYE KUJIAMINI WAMESHINDA). 

WIMBO HUO ULIELEZEA MAISHA YA MADHILA CHINI YA UTAWALA WA WABELGIJI KIPINDI AMABAPO UHURU ULIBADILIKA NA KUELEKEA KWENYE VURUGU.

KABASELE ALITOA KIBAO KINGINE ‘TOYOKANA TOLIMBISANA NA KONGO’ (WENYE MAANA TUELEWANE NA TUSAMEHE YALIYOPITA) UKIHIMIZA KUUNGANA WAKONGOMANI.

MWAKA 1960 KABASELE  ALIREKODI KIBAO KILICHOJULIKANA ‘OKUKA LOKOLE’ AMBACHO NI KWA HESHIMA YA MWANAMUZIKI ‘LOUIS ARMSTRONG’ (SATCHMO) AMBAYE ALITEMBELEA KONGO KWA ZIARA ILIYODHAMINIWA NA SERIKALI YA AMERIKA.

MWAKA 1961 KUNDI LA AFRICAN JAZZ LIKIONGOZWA NA JOSEPH KABASELE LILIFANYA ZIARA NDEFU KATIKA NCHI ZA AFRIKA MAGHARIBI NA KUSAMBAZA MTINDO WAO ILIOKUWA UMECHANGANYA MAHADHI YA KIAFRIKA.

KWA WASIKILIZAJI WA CHANA, NIGERIA, IVORY COAST, SIERRA LEONE NA GUINEA ILILETA ATHARI KUBWA KWA WANAMUZIKI WA HUKO. KWA MFANO BENDI YA BEMBEYA JAZZ YA NCHINI GUINEA, ILIWEZA KUFAIDIKA KWA ZIARA HIYO YA KABASELE YA MWAKA 1961 NA KUWEZA KUZALIWA MUZIKI MCHANGANYIKO WA AFRIKA MAGHARIBI NA LATIN AMERIKA KWA KUPATIKANA MITINDO YA HIGH-LIFE, JUJU NA AFRO-BEAT.


KABASELE BAADAYE ALIIBUKA NA KUWA KIONGOZI MKALI, TABIA AMBAYO ILIPELEKEA WANAMUZIKI WOTE KUHAMA KATIKA BENDI YA AFRICAN JAZZ MWAKA 1963.

ALIJIUNGA NGUVU NA KUSHIRIKIANA NA MWIMBAJI JEAN BOMBENGA. BOMBENGA ALIKUWA MWANAFUNZI WAKE ALIYEKUWA KATIKA BENDI YA VOX AFRICA.

KUNDI HILO LA VOX AFRICA MARA NYINGINE LILITAMBULIKA KAMA AFRICAN JAZZ. 

HATA HIVYO HALIKUFANIKIWA KUFIKIA KIWANGO CHA ILIYOKUWA AFRICAN JAZZ HALISI.

BAADA YA KUNDI HILO KUFANYA KUREKODI KWAO PAMOJA NA MAONESHO KUWA MACHACHE, LILIKUFA MWAKA 1969.

BAADAYE KABASELE AKAFANYA SAFARI YA KWENDA ULAYA KUREKODI AKIWA NA KUNDI LA WANAMUZIKI WALIKUWEPO STUDIO NA KULIPA JINA ‘AFRICAN TEAM’.

KUNDI HILO LILIKUWA NA WANAMUZIKI, WAPULIZAJI WA SXOPHONE, MKAMERUNI MANU DIBANGO NA JEAN SERGE ESSOUS TOKA KONGO BRAZZAVILLE. 

ALIKUWEPO PIA MPIGA FLUTI MCUBA DON GONZALO AMBAO KWA PAMOJA WALICHEZA MIONDOKO YA AFRO-LATIN JAZZ.


MWANZONI  MWA MIAKA YA 1970, KABASELE AKAWA RAISI WA CHAMA CHA HAKI MILIKI CHA KONGO KINSHASA (SONEKA).

AIDHA ALIONEKANA JUKWAANI MARA CHACHE SANA KUTOKANA NA MARADHI YA ‘HYPERTENSION’ SUGU(SHINIKIZO LA DAMU) AMBAYO YALIMUANDAMA SANA.

ALIWAHI KWENDA PARIS MARA MBILI KWA MATIBABU AMAKO ALIKUWA AKIPATA NAFUU YA MUDA.

MWAKA 1980 KABASELE ALITUNIKIWA NISHANI YA ‘MWALIMU MKUU’ WA MUZIKI WA ZAIRE NA UMOJA WA WANAMUZIKI – UMUZA.

LAKINI KWA MAPENZI YA MUNGU, MIAKA MITATU BAADAYE FEBRUARY 11, 1983 KABASELE  AKAFARIKI  DUNIA AKIWA JAMHURI YA KIDEMOKRASIA YA KONGO.

KABASELE ANAKUWA MMOJA WA WANAMUZIKI WAKUBWA WA KARNE YA ISHIRINI. ALIKUWA NA SAUTI PAMOJA NA STAILI KIGEZO, AMBAYO WAIMBAJI WOTE WA KONGO WANGEWEZA KUPIMWA KWA HIYO. BENDI YAKE YA AFRICAN JAZZ ILIKUWA NI MFANO KWA KILA KUNDI LA BENDI ZA WAKONGO WALIOFUATIA.

MCHANGO WAKE KATIKA MUENDELEZO WA RUMBA LA KONGO ULIWAFANYA WAKONGO WOTE KUMWITA ‘BABA WA MUZIKI WA KONGO’.

MUNGU AIPUMZISHE ROHO YAKE PAHALA PEMA PEPONI, AMINA.


 MWISHO.



MJUE "JIM REEVES" ALIYETAMBA KATIKA ULIMWENGU WA MUZIKI


MJUE "JIM REEVES" ALIYETAMBA KATIKA ULIMWENGU WA MUZIKI

Hapana shaka watu wazima wenye umri wa mkubwa kama wangu, ukitamka jina la Jim Reeves, unakuwa umewakuna vilivyo.

Alikuwa ni mwanamuziki wa Kimarekani aliyejikita katika miondoko ya muziki wa ‘Country’ na muziki wa kawaida kama  mtunzi haklikadhalika uimbaji.

Reeves aliweza kuweka rekodi ya muziki wake ukupanda chati toka miaka ya 1950 hadi ya 1980.   

Muziki wake ukawa maarufu na kujulikana kama mwanamuziki wa midundo ya ‘Nashville’ (ambayo ni mchanganyiko wa muziki wa zamani wa country na ule wa kisasa). 

Wasifu wa nguli huyo unaonesha kuwa  jina lake halisi alikuwa ikiitwa
James Travis aka “Jim” Reeves aliyezaliwa Agosti 20, 1923 Reeves amezaliwa katika kitongoji cha Galloways huko Texas, nchini Marekani.

Alitambulika kama ‘Muungwana Jim’ na nyimbo zake ziliendelea kupanda chati kwa miaka kadhaa hata baada ya kifo chake.
Reeve alikuwa akitoka katika jamii ya watu waliokuwa nje ya mji karibu na Carthage. Alifariki Julai 31, 1964 akiwa na umri mdogo wa miaka 40 katika ajali ya ndege binafsi.

Yeye alikuwa mwanachama wa muziki wa ‘Country’ na pia ule wa Texas Country Halls of Fame.

Jim alifanikiwa kupata nafasi ya kusomamsomo ya juu ‘Scholarship’ ambapo alijisaljili kusomea masuala ya kuhutubia na maigizo.

Baada ya miezi sita katika masomo hayo, aliachana nayo akaamua kwenda kufanya kazi katika yadi ya kutengeneza Meli huko Houston.

Licha ya kuwa na weledi katika muziki Reeves pia alikuwa mwanariadha aliyewahi kuchezea ligi za Semi-Professional kabla hajaingia mkataba na St. Louis Cardinals, timu ya shamba. Mwaka 1944 alicheza kama right-handed Pitcher. 

Aidha alicheza ligi ndogo kwa miaka mitatu kabla hajaumia na kupata maumivu katika misuli iliyohitimisha juhudi zake za kuendelea na michezo.
Reeves alianzia kufanya kazi kama mtangazaji wa radio. 

Kila wimbo umalizikapo kuupiga radioni, yeye akawa anaimba wimbo huo.

Mwishoni mwa miaka ya 1940, aliingia mikataba na baadhi ya Makampuni madogo ya kurekodi, huko Texas lakini hakupata mafanikio. 

Muziki wa Magharibi ulimfanya kuhamasika sana hususani alipokuwa akiwasikia wanamuziki kama Jimmie Rodgers na Moon Mullicann. 

Waimbaji wengine maarufu wakati huo aliokuwa akiwatamani ni akina Bing Crosby, Eddy Arnold na Frank Sinatra.

Mapenzi hayo makubwa katika muziki yalimpelekea kuwa mwanachama wa bendi ya Moon Mulican.

Jim aliweza kufanya mitindo ya mwanzoni za bendi ya Mullican, nyimbo zake kama ‘Each Beat of My Heart’ na ‘My Heart’s Like a Welcome Mat’ mnamo miaka ya 1940 mwishoni na mwanzoni 1950.
 
Reeves aliweza kuimba nyimbo za ‘Mexican Joe’ ambazo zilishika namba moja mwaka 1953.

Kutoka mwaka 1955 mpaka kuendelea mwaka 1969 Reeves nyimbo zake ziliendelea kushika ‘ukanda’ hata baada ya yeye kufariki.

Nyimbo zake za kwanza za ‘Country’ zilizompa mafanikio zilikuwa ni pamoja na ‘I Love You’ alouimba akishirikiana na Ginny Wright, na ‘Mexican Joe’ ‘Bimbo’.
 
Nyimbo nyingine zilizotolewa na Fabor Records na Abbott Records ilitoa albam yake ya kwanza Novemba, 1955 iliyojulikana ‘Jim Reeves Sings’. 

Mapema mwaka 1955, Reeves alisaini mkataba wa miaka 10 na Kampuni ya RCA Victor chini ya Steve Sholes, ambaye alitoa rekodi za kwanza za Reeves akitumia Kampuni ya RCA na pia akaingia mkataba na Elvis Presley na kampuni hiyo hiyo mwaka huo huo.

Alipokuwa akirekodi mwanzoni akiwa na  Kampuni ya RCA, Reeves bado alikuwa anaimba kwa staili ya sauti ya juu ambapo ilionekana ndio kipimo cha nyimbo za ‘Country’ Wanamuziki wa Magharibi kwa wakati huo. 

Baadaye Jim alianza kupunguza sauti yake wakati akiimba na kutumia ‘Pitch’ ya chini akiimba huku midomo yake ikikaribia kugusa kipaza sauti, ingawaje waliokuwa wanamrekodi (RCA) walikuwa wanailalamikia hali hiyo. 

Mwaka 1957 kwa maelekezo ya ‘Produysa’ wake Chet Arkins alitumia mtindo huo katika toleo la wimbo wa maonesho wa ‘Penzi lililopotea’ uliokusudiwa uimbwe na mwimbaji wa kike.

Katika kipindi chote miaka yote ya 1950 na hadi 1960 mwanzoni, Jim Reeves aliachia nyimbo zake kali zizoshika ‘chati’ za ‘Anna Marie’ na  ‘Blue Boy’ No. 2 za mwaka  1958.

 Alifyatua kibao kingine cha ‘Billy Bayo’ mwaka 1959 na  ‘He will have to go’ wa mwaka 1960., ‘Adious Amigo’ (namba mbili, 1962), ‘Welcome to my World’ (namba mbili, 1964) na ‘I guess I’m crazy’ (namba moja kwa wiki saba, 1964).
Jim Reeves  pia alikuwa na kikosi na idara ya nyimbo za dini katika jukwaa lake.
Wimbo wake, ‘Danny Boy’ akijitambulisha kwamba wazazi wake wametokea Irish. Wimbo ‘But You Love Me Daddy’ ukirekodiwa wakati mmoja akiwepo ‘Steve’ mtoto wa miaka minane wa mpiga gitaa la besi, Bob Moore, ulikuwa katika ishirini bora huko Ulaya miaka kumi Baadaye. 

Rekodi zake mara nyingi zilikuwa na utamanifu wa kipekee, kama ‘I Love you Because’ (ulishika namba 5) na ‘I won’t forget You’ (namba 3) zilikuwa katika chati huko UK kwa wiki 39 na 25 mfululizo.

Reeves alikuwa amesaidia sana kuanzisha staili mpya ya muziki wa ‘Country’ akitumia ‘violin’ na ‘mpangilio wa kupendeza wa background ikijulikana kama ‘Nashville’ sound.   

Alipata umaarufu kama muimbaji wa kiume mwenye sauti ya kupendeza na nzito kiasi, yenye madaha. 

Nyimbo kama ‘Adios Amigo’ ‘Welcome to My World’ na ‘Am I Losing You’ zinaonyesha hili. 

Nyimbo zake za Chrismas zikijirudia rudia na kupendwa sana hasa zikiwa ni pamoja na ‘Chrismas’ ‘Blue Chrismas’ na ‘An Old Chrismas Card’.
 
Hali kadhalika Jim Reeves amekuwa hodari kwa kuukweza na kuzipa maarufu nyimbo nyingi za ‘Injili’ kama ‘We Thank Thee’ ‘Take My Hand, Precious Lord’ ‘Across The Bridge’ ‘Where We’ll Never Grow Old’ na nyingine nyingi.

Reeves aliibua mafanikio makubwa kwa utunzi wa Joe Allison, ‘He’ll have to Go’. 

Kwa kweli kulikuwa na mafanikio makubwa kwa muziki huu wa kawaida na wa ‘Country’ ambapo ulimpatia ‘Platinum Record’ ambayo ilitolewa mwishoni mwa mwaka 1959 na ilifanikiwa  kuwa namba moja katika gazeti la ‘Billboard’. 

Katika nyimbo za ‘Country’ ambazo zili ‘hit’  kuanzia 08/February, 1960 na kuendelea kwenye chati kwa wiki 14 mfululizo hii moja wapo.

Mwana historia wa muziki wa Country, Bill Malone alionesha kwamba ni katika namna nyingi Reeves aliendeleza utamu na ubora katika   muziki wa ‘Country’ kimpangilio na ‘melodi’ safi na ujumbe unaogusa  mioyo ya watu. 

Kwa nyongeza, Malone alimsifia Reeves kwa staili yake ya kuimba ambayo anaishusha chini sauti yake, inakuwa kama ya kubembeleza na ndio maana watu wengi wanatamka kwamba Jim Reeves ni muimbaji mwenye sauti ya mguso.

July 31, 1964, Reeves na mshirika mwenzake wa kibiashara, Meneja Dean Manuel waliondoka Batesville, Arkansas kupitia Nashville wakitumia ndege ya injini moja akiwa Reeves anaendesha.

Wawili hao walikuwa wamepata ‘dili’ ya kununua shamba huko Deadwood Texas, Kaskazini mwa Galloway ambayo ni sehemu aliyozaliwa Reeves.

Wakati wanapaa juu kwa ndege akiwa na  Brentwood, Tennessee, walikutana na dhoruba ya upepo mkali na mvua kubwa.

Katika uchunguzi ilionekana ndege hiyo ndogo ilinaswa katika dhoruba na Reeves alipata mstuko ikaanguka na wao wakafariki. 

Mjane wa marehemu, Mary Reeves  alianzisha uvumi kwamba Reeves alikuwa akiendesha juu chini na aliongeza spidi ili kukwepa  dhoruba.

Hata hivyo kulingana na Larry Jordan, maelezo ya mjane wake kwamba Reeves alikuwa anaendesha chini juu si sahihi.
Kutokana na watu walioiona ajali hiyo jinsi ndege ilivyoanguka na  maelezo yaliyomo kwenye tape iliyorekodi mwenendo wa ndege.

Pia maelezo ya ripoti ya ajali, kwamba Reeves alikata kushoto katika jitihada zake za kuipata Franklin road ili afike uwanja wa ndege aweze kutua.  

Katika jitihada yake hiyo  akazidi kuelekea kule kwenye mvua kubwa.

Katika kuhangaika ili akakipate kiwanja ili kutua,  spidi ya ndege ikawa ipo chini hivyo akaikwaza ndege. 

Reeves alitegemea zaidi hisia zake katika kumuongoza na hakutumia maarifa  aliyofundishwa chuoni kuikabili hali kama hiyo. 

Baada ya masaa 42 mabaki ya ndege yalionekana ikiwa  mbele, yaani usoni pamoja na injini vimejikita ardhini.  Reeves na mwenzake walikutwa tayari wamekwisha fariki.

Jim Reeves alizikwa katika kipande cha ardhi maalum ubavuni mwa ‘Highway 79’ Texas.

Licha ya kufariki Jim Reeves bado umaarufu wake haukupotea, kwa hakika mauzo ya kazi zake yameongezeka baada ya kufariki.
  
Mjane wake, Mary Reeves (70) alifariki katika siku ya ‘Veteran’ Tarehe Novemba 11, 1999, iliripotiwa kuwa amekufa akiwa peke yake katika nyumba ya kuuguza wagonjwa. 

Hata hivyo mazishi yake yalipangwa kwa watu wachache tu wa karibu ikiwa hii ni agizo la aliyekuwa mumewe wa pili Tery Davis.

Tangu kipindi cha kifo cha Jim Reeves kulipotokea, Mary alipatwa na matatizo ya kuugua kabla hayajamzidia. 

Alikuwa ni kiungo muhimu katika kuuweka muziki wa Reeves na kumbukumbu zake alizifanya kuwa hai.

Kutokana na Mary Reeves Davis kushindwa kutokana na ugonjwa kuzisimamia mali za Jim Reeves ziliuzwa kwa ‘United Show of America’ mwaka 1997 kwa thamani  ya Dola za Kimarekani milioni 7.3
Jim Reeves aliwekwa kwenye kundi la mwimbaji Nyota wa Kiume ambaye ametokeza katika midundo ya ‘Nashville Sound’.
Sauti yake laini ya kidume yenye madaha imeendelea kusikika hadi wakati leo.

Mwisho.