Saturday, October 10, 2015

JE, UNAFAHAMU KAMA ILIKUWEPO BENDI YA WANAWAKE NCHINI?



JE, UNAFAHAMU KAMA ILIKUWEPO BENDI YA WANAWAKE NCHINI? 

Ule usemi kwamba “Wanawake wanaweza” inaelekea kwamba ulikuwepo tangu zamani. Mnamo miaka ya 1960, hapa nchini ilianzishwa bendi ya wanawake watupu ikiwa na jina la ‘ Women Jazz Band.
Bendi hiyo haikufahamika sana kwa kuwa haikudumu sana na pia nyimbo zake hakuendelea kupigwa katika vituo vya redio licha ya kuvirekodi katika redio ya taifa wakati huo ya Radio Tanzania Dar es Salaam(RTD).
Kama ilivyo kwa historia kwamba huwa haifutiki, inaeleza kuwa mwaka 1965, kundi jipya la aina yake lilianzishwa nchini humu lilikuwa ni bendi ya akina mama watupu. Bendi hiyo iliitwa Women Jazz.
Akina mama hao wengine walikuwa ni wafanyakazi wa Idara ya Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali (Government Press), ambao walijichaguana wakaanza kuhudhuria mafunzo ya muziki chini ya yule mwanamuziki mahiri Mzee Mayagilo.
Mayagilo kipindi hicho alikuwa kiongozi wa kitengo cha muziki Brass band katika Jeshi la Polisi, waanza mazoezi kwa nguvu.

Bendi hiyo ilikuwa chini ya Umoja wa Vijana wa TANU (TANU Youth League) wakati ule. Sasa ni UVCCM.
Kina mamam hao walipokuwa wakianza shughuli hiyo walikuwa hawana ujuzi wowote wa katika muziki. Kutokana na jitihada zao wakajitengenezea utaratibu wa kuanza kufanya maonesho yao hasa kwenye hafla za serikali na Chama tawala cha TANU wakati huo.
Dhamira yao ilitimia Mei 31, 1966 ambapo bendi yao iliingia katika studio za RTD zilizopo jijini Dar es Salaam na kurekodi nyimbo zao sita.
Nyimbo hizo zilikuwa za Tumsifu mheshimiwa, Leo tunafuraha, Mwalimu kasema, Women Jazz, Sifa nyingi tuwasifu viongozi na TANU yajenge nchi.
Nathubutu kutamka kwamba nyimbo za akina mama hao hazifahamiki kwa kizazi hiki kwa kuwa hazisikika zikipigwa katika kituo cha redio chochote hata TBC taifa iliyo na maktaba kubwa ya muziki!
Ka mantiki hiyo basi itakuwa ni busura zikatumika kwa uongozi bora wa TBC Taifa, kuzikumbuka kupiga nyimbo hizo ili kuweka changamoto kwa kizazi hiki hususani kwa akina dada wanao chipukia kimuziki.
Women Jazz alikuwa ikiundwa na akina Mary Kilima, Juanita Mwegoha, Rukia Hassan na Siwema Salum ambao walikuwa waimbaji katika bendi hiyo.
Wengine ni Kijakazi Mbegu aliyekuwa akilicharaza gitaa la solo, Mwanjaa Ramadhani alikuwa akiliungurumisha gitaa zito la besi na Chano Mohammed, aliyekuwa akipiga gitaa la kati la rhythm.
Kwa upande wa ‘mdomo wa bata’ walikuweapo Tatu Ally na Anna Stewart waliokuwa wakipuliza Alto Saxophone wakati Mina Tumaini na Rukia Mbaraka wakipuliza Tenor Saxophone.
Mama aliyejulikana kwa jina la Lea Samuel alikuwa akichangaya Bongos, wakati huohuo Josephine James alikuwa akidunda  drums.
Miaka hiyo kulikuwa na zana nyingi za muziki tofauti na miaka hii. Kulikuwepo na chombo kikiitwa Maracass kilichokuwa ambacho katika bendi hiyo kilichezwa na Zainabu Mbwana wakati kile cha Timing alikuwepo Tale Mgongo.
Kwa wale wasioijuwa ama kukumbuka historia ya chama cha TANU, kirefu chake ni Tanganyika African National Union. Hicho ndicho kilikuwa chama kilichotawala Tanganyika na Tanzania hadi muungano wa chama hicho na Chama cha Afro-Shirazi cha Zanzibar, vilipounda Chama Cha Mapinduzi (CCM) mwaka 1977.
Chama cha TANU kilianzishwa 7 Julai, 1954, kabla yake kulikuwepo na chama cha Tanganyika African Association (TAA).
TAA ilikuwa na mwelekeo wa kitamaduni zaidi ya siasa. Mwenyekiti wa kwanza wa TANU alikuwa Julius Kambarage Nyerere.
TANU ilikuwa ikishinda kila uchaguzi chini ya utawala wa kikoloni ikawa chama cha kuongoza Tanganyika hadi ilipopata uhuru wake mwaka 1961.
Katiba ya Taifa ya mwaka 1962 ilifanya TANU kuwa chama cha pekee nchini ikifuata mfano wa nchi za kijamaa zenye muundo wa siasa ya chama kimoja.
Bendi ya Women Jazz ilipata umaarufu kiasi cha kuanza kufanya safari nje ya Tanzania, na kuweza kufanya maonesho katika miji ya Nairobi na Mombasa, baada ya kutembelea miji kadhaa hapa nchini.
Baada ya waaamuziki wa bendi hiyo kujiona hawapati faida yeyote kutokana na mapato ya bendi yao, wakiwa katika maandalizi ya kufanya ziara ya kwenda nchini China, bendi hiyo ilisambaratika.
Hii chamngamoto kwa Wanawake wa hapa nchini kuiga mfano wa wenzao waliowatangulia wakathubutu, wakafanikiwa kuwa na bendi yao.

Mwisho.




BENDI YA MLIMANI PARK ILIVYOLITEKA JIJI LA DAR ES SALAAM



BENDI YA MLIMANI PARK ILIVYOLITEKA JIJI LA DAR ES SALAAM

KWA KAWAIDA HISTORIA YA JAMBO LOLOTE HUWA HAIFUTIKI. HISTORIA YA BENDI YA MLIMANI PARK ORCHESTRA INAELEZA KUWA MWANAMUZIKI MWANZILISHI WA BENDI HIYO ALIKUWA ABEL BARTAZAR ALIYEUNGANA NA WANAMUZIKI WANANE WALIOIHAMA BENDI YA DAR INTERNATIONAL WAKAENDA KUIJENGA VILIVYO MLIMANI PARK ORCHESTRA  MWAKA 1978.

WANAMUZIKI HAO NI PAMOJA NA ALIYEKUWA MTAALAMU WA KUPIGA ALA ZOTE ZA MUZIKI, MICHAEL ENOCK ‘KING’, JOSEPH BENARD, JOSEPH MULENGA, ABDALAH GAMA, COSMAS CHIDUMULE, MACHAKU SALUM NA HABIB JEFF. 

BENDI YA MLIMANI PARK ORCHESTRA ILIKUWA CHINI YA UONGOZI WA TANZANIA TRANSPORT AND TAX SERVICES (TTTS), IKIWA NA MASKANI YAKE PALE MLIMANI CLUB MITAA YA MWENGE JIJINI DAR ES SALAAM.

MLIMANI BAADAE MWAKA 1983, ILICHUKULIWA KUWA CHINI YA SHIRIKA LA MAENDELEO YA DAR ES SALAAM (DDC), BAADA YA  WALIOKUWA WAMILIKI TTTS  KUFILISIKA.

BENDI HIYO IKAANZA KUITWA KWA JINA LA DDC MLIMANI PARK ORCHESTRA IKIWA CHINI YA WANAMUZIKI WAASISI, MUHIDIN MAALIM GURUMO, ABEL BALTAZAR, HASSAN REHANI BITCHUKA, AMBAO WALITOKEA JUWATA JAZZ BAND HUKU COSMAS THOBIAS CHIDUMULE, MICHAEL ENOCH ‘KING MICHAEL’ NA MPIGA GITAA LA SOLO MAHIRI, JOSEPH BATHOLEMEO MULENGA.

WANAMUZIKI HAO WALICHUKULIWA KATIKA BENDI YA DAR INTERNATIONAL.

ALIKUWA GWIJI MUHIDIN GURUMO ALIYEBUNI MTINDO WA SIKINDE NGOMA YA UKAE, ALIOUELEZEA KUWA NI MTINDO WA NGOMA ZA UTAMADUNI WA KABILA LAKE LA KIZARAMO.

MTINDO HUO HADI SASA NDIO UNAOTAMBA NA WAKATI MWINGINE HUTUMIWA NA WAPENZI KUITA SIKINDE KAMA JINA LA BENDI.

BENDI HIYO ‘ILIACHIA’ VIBAO VINGI VILIVYOTAMBA NA HADI LEO VINASIKIKA VIKIPIGWA NA BAADI YA VITUO VYA REDIO HAPA NCHINI.

BAADHI YA VIBAO HIVYO NI PAMOJA NA SAUDA, MV MAPENZI, NEEMA, USITUMIE PESA KAMA FIMBO, MUME WANGU JERRY, CLARA, HIBA NA MATATIZO YA NYUMBANI.

NYIMBO ZIGINE ZILIKUWA ZA MAJIRANI HUZIMA REDIO, NIDHAMU YA KAZI, KASSIM AMEFILISIKA,TALAKA YA HASIRA, HADIJA, BARUA TOKA KWA MAMA, CELINA, EDITHA NA FIKIRI NISAMEHE.

BENDI HIYO ILIKUWA NA WATUNZI WENGI MNO KIASI KWAMBA WALIWEZA KUTUNGA NA KUIMBA NYIMBO ZINGINE ZAIDI ZIKIQWEMO ZA POLE MKUU MWENZANGU, DIANA, PESA, HATA KAMA , BUBU ATAKA SEMA, MNANIONESHA NJIA YA KWETU, TANGAZIA MATAIFA YOTE, MTOTO AKILILIA WEMBE, NALALA KWA TABU NA DUNIANI KUNA MAMBO. 

ZINGINE ZAIDI NI KIU YA JIBU, DUA LA KUKU, NAWASHUKURU WAZAZI, PATA POTEA, NELSON MANDELA, UZURI WA MTU, MDOMO HUPONZA KICHWA, TAXI DRIVER, TUCHEZE SIKINDE, CONJESTA NA NYIMBO NIYNGINE NYINGI.


DDC MLIMANI PARK ORCHESTRA ILIKUWA NA WANAMUZIKI WENGI WENYE VIPAJI TOFAUTI AKINA MICHAEL ENOCK, JOSEPH BENARD, JOSEPH MULENGA, ABDALAH GAMA, COSMAS CHIDUMULE, MACHAKU SALUM, HABIB JEFF NA MUHIDIN MAALIM GURUMO.

WENGINE WALIKUWA HASSAN REHANI BITCHUKA, ABEL BARTHAZAR, HENRY MKANYIA, FRESH JUMBE, HUSSEIN JUMBE, BENNO VILLA ANTHONY, TINO MASINGE 'ARAWA', HASSAN KUNYATA, FRANCIS (NASSIR) LUBUA, MAALIM HASSAN ‘KINYASI’, NA ABDALLAH GAMA.

SAFU HIYO ILIKUWA PIA NA MAX BUSHOKE, MUHARAMI SAID, KASSIM MPONDA, JULIUS MZERU, SAID CHIPELEMBE, ALLY JAMWAKA, MACHAKU SALUMNA  ALLY YAHAYA.

WENGINE WALIOENEZA SAFU HIYO NI PAMOJA NA SHABAN LENDI, JOSEPH BERNARD, JUMA HASSAN TOWN NA WENGINE WENGI. SHIRIKA LA MAENDELEO DAR ES SALAAM BAADE LIKAJITOA KUIFADILI BENDI HIYO JAPO ILIWAACHIA VYOMBO VYOTE VYA MUZIKI ILI WAWEZE KUJITEGEMEA. WAKABADILISHA JINA LA BENDI NA KUWA MLIMANI PARK ORCHESTRA. BENDI HIYO BADO INALITIKISA JIJI LA DAR ES SALAAM WAKIWA NA MAKAO YAO MAKUU KWENYE UKUMBI WA DDC KARIAKOO JIJINI DAR ES SALAAM.

B

Thursday, October 8, 2015

UNAMKUMBUKA FRANKLIN BOUKAKA?



UNAMKUMBUKA FRANKLIN BOUKAKA?


Ule usemi usemao kuwa “Maji hufuata mkondo” unajionesha wazi kwa mwanamuziki Frankin Boukaka aliyerithi  mikoba ya baba yake.

Alikuwa ni mtoto wa Aubin Boukaka aliyekuwa mwanamuziki wa kundi la ‘The Gaiety’ wakati mkewe Yvonne Ntsatouabaka alikuwa  mshereheshaji (MC) maarufu  kwenye misiba na pia alikuwa mwanamuziki muimbaji.

Mara baada ya kuzaliwa Oktoba 10, 1940, alipewa jina la François Boukaka baadae akajulikana kama Franklin.

Alikuwa mtoto wa kwanza katika familia ya watoto wanane wavulana watatu na wasichana watano.

Franklin Boukaka alijongezea umaarufu zaidi nchini mwake pale alipojiunga na wenzie waliotaka kuipindua serikali ya Kongo Brazzaville wakati huo ikiwa chini ya uongozi wa rais Marien Ngouabi.

Elimu yake alipata katika shule mbalimbali nchini kwake Kongo Brazzaville. Franklin  alianza kujishighulisha na mambo ya muziki 1955 katika kundi lililojiita Sexy Jazz.

Kundi hilo lilikuwa likiongozwa na Miguel Samba, baadae akaanzisha kundi la Negro Band.

Hatimae katika safari yake ya muziki akaungana na wakali wengine kama  Edo Clary Lutula, Jeannot Bombenga, Tabu Ley ,Mutshipile "Casino", André Kambite " Damoiseau ",  Papa Bouanga, Charles Kibongue katika lile kundi maarufu la African Jazz, sauti ya Franklin imo katika nyimbo kama  Mwana mawa , Catalina cha cha na Marie José zilizotungwa na Tabu Ley.

Mwaka 1959 kundi la African Jazz lilimeguka baada ya wanamuziki wengine walipohamia katika jiji la Brussels nchini Ubelgiji wakifuatana na wanasiasa wa Kongo kwenye mazungumzo ya awali ya uhuru wa Kongo.

Wanamuziki waliobaki akiwemo Jeannot Bombenga,  ila Tabu Ley wakajiunga na kuanzisha kundi jingine lililotingisha nchi lililoitwa Vox Africa.

Waimbaji wakati huo wakiwa ni akina Franklin Boukaka na Jeannot Bombenga.

Baada ya hapo Franklin akaaliacha kundi hilo na kurudi kwao Brazzaville ambako  mwaka 1962, akawa mmoja wa wanamuziki wa bendi ya Cercul Jazz. 

Bendi hiyo ilianza miaka ya 1950, ikiwa chini ya Chama cha vijana kilichokuwa kikipata ufadhili wa serikali ya Ufaransa. 

Chama hicho kiliitwa Cercule Culturel de Bacongo. 
Hatimae Boukaka alikuja kuwa kiongozi wa chama hicho na kikawa na umaarufu wa mkubwa. Wimbo wa bendi hiyo ‘Pont Sur le Congo’ (Daraja juu ya Mto Congo), ulikuwa una hamasisha kuunganika kwa Kongo Leopoldville (Kinshasa) na  Kongo Brazzaville baada ya nchi hizo kupata uhuru.

Kufikia hatua hiyo wimbo huo ukapata umaarufu kuliko nyimbo zote za bendi hiyo.

Baadae Franklin akiwa na gitaa lake kavu akaanzisha kikundi ambacho kilikuwa na wapiga marimba wawili akaweza kufanya ziara kadhaa hata nje ya nchi yake na kundi hilo.

Mwaka 1970 Boukaka  aliweza kurekodi nyimbo 12 zilizopangwa vyombo na Manu Dibango. Nyimbo za Nakoki na Le Bucheron ndipo zilipopatikana. 

Baada ya hapo Franklin alijiunga na wenziwe waliotaka kuipindua serikali ya Kongo Brazzaville, wakati huo ikiwa chini ya uongozi wa rais Marien Ngouabi.

Jaribio hilo lililofanyika tarehe 22 February 1972 lilishindwa na siku chache baadae kifo cha Boukaka kilitangazwa.

Mungu ailaze roho yake pahala pema pepeni, Amina.

Mwisho.