TUIKUMBUKE
TABORA JAZZ
Bendi ya Tabora Jazz
ilikuwa na makazi yake mjini Tabora ikipiga muziki wake katika ukumbi wa
nyumbani wa Lumumba.
Nyimbo nyingi za bendi
hiyo zilipigwa mno kwenye kumbi za starehe pamoja na kituo cha Radio Tanzania
Dar es Salaam(RTD) na vituo vingine vya Radio vya Afrika ya mashariki.
Tabora Jazz ilitamba
kwa mitindo yake ya za Segere Matata, Segua Segua na Mambo Mileka.
Mji wa Tabora
unaelezwa kwamba ulianza kupata burudani za muziki wa dansi hata kabla ya
chama cha TANU hakichaanzishwa.
Kwa mujibu wa Hassan
Athuman ambaye aliyekuwa mwanamuziki wa enzi hizo akipiga gita la solo katika
bendi za Tabora Jazz, Kiko Kids, Nyanyembe Jazz na Milambo Jazz ‘Sona
Sona’ kwa nyakati tofauti.
Alisimulia kuwa
mnamo mwaka 1953 ilianzishwa bendi ya muziki wa dansi iliyopewa jina la Staff
Jazz ikiongozwa na Hamisi Wampa.
Vyombo vya muziki vya
bendi hiyo vilinunuliwa na mfadhili mmoja wa kabila la Kimmanda’ toka nchini
Malawi, aliyenunua vyombo hivyo wakati huo akiwa mfanyakazi wa Bomani.
Staff Jazz ilikuwa na
mdhamini akiitwa mwalimu Hasanari. Waanzilishi wake walikuwa akina Hamisi
Ali Songo ‘ngoma kubwa’ , Hamisi Ngege alikuwa mpiga ngoma ndogo, Dani
Kafumu na Nzige wapulizaji tarumbeta, Akbaru Hasanari Dremsi ‘ngoma
kubwa’ Joseph Kayombo ‘bambo’ mwimbaji, Moshi ‘marakasi’, Saidi ngoma
ndogo’ Haji Sungura ‘mlangoni’, Swedi Mandanda 1953/56/58 Hamisi Issa
‘’trarumbeta’ na ryhtm. Hii ilikuwa kati ya miaka ya 1953 hadi 1958.
Wanamuziki wengine
walikuwa akina Abdi Fundi upande wa ‘sax’ Athuman Tembo kuimba na ‘solo’
Zakaria Tenda wema(mwimbaji) Sylvester Chifunda ‘mwimbaji’ Juma Athumani
‘drums’ aka Juma Lumango na Mlekwa Suleimani mmoja wa viongozi. Rajabu Risasi
upande wa gita la besi.
Staff Jazz ilikuwa
ikipiga muziki kwenye ukumbi wa baa ya Rufita ambayo baadaye ukabadilishwa na
kuwa Lumumba uliyokuwa katika kona ya barabara za Rufita na Kapembe,
katikati ya mji wa Tabora.
Bendi hiyo kwa sababu
ambazo hazikuainishwa, mwaka 1954 ilisambaratika.
Busara na hekima za
Hamis Alli Songo zilimfanya aifufue bendi hiyo mwaka 1956 kwa jina lingine la
Tabora Jazz.
Yaelezwa kuwa Mlekwa
Selemani aliyekuwa shabiki mkubwa wa bendi ya Kiko Kids, akajiunga na Tabora
Jazz na kuwa mmoja wa viongozi wa bendi hiyo.
Mwaka 1958 bendi hiyo
ilichukuliwa kwenda Kanda ya Ziwa kwa ajili ya kuhamashisha nguvu ya chama cha
TANU wakiongozana na viongozi wake Rashid Mfaume Kawawa, Mzee
Herman Pacha, mama Mosi Tambwe na mumuwe Abdallah Selemani.
Bendi iliporudi
Rashidi Hazuruni mwaka 1959 aliondoka kwenda Dar es Salaam akajiunga na Quban
Branch iliyokuwa ikiongozwa na Mzee Mwaipungu.
Kati ya mwaka 1960 na
1961 bendi ilikuwa na wapigaji gita la solo wawili akina Abdi Fundi na Matata.
Mwaka uliofuatia Athumani Tembo akaongezeka katika ukung’utaji wa gita hilo.
‘Maisha ni kuhangaika’
usemi huu ulijionesha wakati Rashidi Hazuruni aliporejea tena kupiga muziki na
Tabora Jazz mwaka 1963.
Tabora Jazz ilisheheni
wanamuziki wengi wakiwemo akina Hamisi Wampa aliyekuwa Kiongozi, Hamisi Alli
Songo na Akbaru Hasanari Dremsi walikuwa wadunda ngoma kubwa, Mambosasa alikuwa
akipiga ukulele (gita la kizamani). Mambosasa ndiye aliyekuwa baba yake mzazi
na Athumani Mambosasa, aliyewahi kuwa mlinda mlango wa Klabu ya Simba.
Said na Hamis Ngege
walikuwa wakipiga ngoma ndogo, Dani Kafundu na Nzige walikuwa
wapulizaji wa tarumbeta wakati Joseph Kayombo ‘Bambo’ alikuwa mwimbaji.
Kwa upande wa marakasi
alikuwemo Moshi, Haji Sungura aliyekuwa mlinzi ‘mlangoni’, Swedi Mandanda
alikuwa mcharazaji wa gita la solo, Hamisi Issa alikuwa akipiga gita la kati
‘rhythm’ na Tarumbeta.
Wanamziki wengine
walikuwa Athumani Tembo kwenye solo, upande wa gita la rhythm walikuwa
Hamis Issa na Fundi Hassan Athumani.
Besi liliungurumishwa
na Kassim Mponda aliyeondoka katika bendi hiyo mwaka 1965 mwishoni, akifuatana
wanamuziki wengine akina Rashidi Hazuruni na Omari Kayanda wakaenda kujiunga na
Western Jazz.
Mwaka 1966 Tabora Jazz
ikapata mpiga solo mwingine aliyejulikana kwa jina la Stan kuziba pengo la
Rashidi Hanzuruni.
Upande wa safu ya
waimbaji walikuwa Atrhumani Tembo, Omari Kayanda , Sylvester Chifunda na Joseph
Kayombo ‘Bambo’
Mpigaji bongos (ngoma
ndogo) alikuwa Juma Athumani ‘kisegeju’ Abdi Fundi alikuwa akipuliza saxophone
’mdomo wa bata’
Kati ya mwaka 1964 na
1965, Tabora Jazz walirekodi nyimbo baadhi yake zikiwa za Ndugu sikilizeni,
Tuambie, Dunia haina mwisho, Mwanawanyeje na nyinginezo.
Mwaka 1967 Kassimu
Kaluwona alikwenda Kigoma na kuweza kuwaleta Wema Abdallah, Hamis
Kitambi, Issa Ramadhani ‘ ‘Baba Watoto’ Mabrushi
Ramadhani
Mgoligwa na Hamisi Mkongo.
Mwaka 1968 Salumu
Luzira akaijunga na Tabora Jazz akitokea Nzega.
Mwaka 1971 Wema
Abdallah akaondoka Tabora Jazz akaenda Western Jazz, nafasi yake ikachukuliwa
na mpiga solo mwingine aliyejulikana ka jina la Kalii, alikitokea Kigoma Jazz.
Kwa kipindi kifupi
Said Mabera na Hassan Rehan Bichuka nao walijiunga na Tabora Jazz wakitokea
Rumonge Jazz.
Shem Karenga aliletwa
na Kassim Kaluwona toka Kigoma, kuja Tabora kujiunga na bendi hiyo Aprili 1972.
Shem baada ya kutua, alishiriki vilivyo katika
utengenezaji wa wimbo wa Dada Asha ambao baadaye
Wimbo wa Dada Asha
uliibwa na bendi ya Sokous Stars ya akina Lokassa ya Mbongo ya nchini Kongo na
kuichakachua ukiwemo wimbo wa Vigeregere uliopigwa na Western Jazz. Pia
mwanamuziki Lita Bembo na vijana
wake wa Stukas nao walikwapua na kuupiga wimbo huo.
Kwa mujibu wa Hassan
Athumani amsema kuwa wimbo wa Dada Asha, mtunzi wake alikuwa askari jeshi
aliyeomba atengenezewe wimbo huo.
Tabu Ley aliiona album
yenye wimbo huo wa Dada Asha akiwa Nairobi na aliinunua akaenda kuiuza nchini
Kongo, Poland na Ubelgiji.
Bendi hiyo baadaye
akajipanga upya kwa kupata damu changa ili kuendeleza muziki wake.
Iliongeza watunzi na
waimbaji wengi akiwemo Msafiri Horoub, Madaraka Morris, Ismail Wangoko na
wengine wengi.
Kwa umoja wao
wakafyatua nyimbo nyingi zilizoweza kuridhisha nyoyo za wapenzi na mashabiki wa
Tabora Jazz. Nyimbo hizo ni Ashura, Helena, Mapenzi ulimi, Visa uache, Lucie
umeniacha, Zabibun na Niambie leo Kaka. Ziningine zilikuwa za Usijifanye Mwewe,
Mariam mpenzi, Zabibu No.2, Sofia mpenzi, Tatu, Serafina, Tamaa yako
na Asha No. 1. Zote hizo zilikuwa zikitamba mno wakati huo. Zingine
ni pamoja na Alhamdulilah, Nashukuru sana, na Dada Asha.
Nyingine ni pamoja na Dada Mwantumu, Ujana una
mwisho, mwisho wake ni uzee. Zingine zilikuwa za Salima, Mapenzi Ulimi, Dada
Remmy na Rukia wajidanganya.
Wanamuziki wengi wanatajwa katika bendi hii ya
Tabora Jazz, baadhi yao wapo hai kama vile Shem Karenga, Ramadhani Mwanangwa
(rhythm) Salumu Luzira na wengine wengi.
Baadhi ya wanamuziki wanaotajwa katika makala
hii wamekwishafariki.
Walio haihaajishughulishi tena na maswala ya
muziki kufuatia umri kuwatupa mkono.
Bendi ya Tabora Jazz
haipo tena katika ulimwengu wa muziki.
Mwisho.