Friday, May 13, 2016

ANGELIQUE KIDJO ASHINDA TUZO YA GRAMMY



 ANGELIQUE KIDJO ASHINDA TUZO YA GRAMMY 

Mwanamuziki wa nchi ya Benin Angelique Kidjo ameshinda tuzo ya Grammy pamoja na wanaharakati watatu kutoka barani Afrika, wametuzwa tuzo ya haki za kibinaadamu mwaka 2016 kwa kusimamia haki na shirika la Amnesty International.

Wengine walioshinda ni pamoja na Yen a Marre wa Senegal, Le Bali Citoyen kutoka Burkina Faso na Lucha kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Katibu Mkuu wa Amnesty International Salil Shetty alitangaza katika taarifa yake kwamba wote wameonyesha ujasiri, shirika hilo la haki za kibinaadamu kwamba wanapigania haki za kibinaadamu kwa kutumia vipaji vyao kuwashiwishi wengine.

Kidjo pia anajulikana kwa kampeni yake kwa uhuru wa kujieleza pamoja na vita dhidi ya ukeketaji.

Mwanamuziki huyo amejiunga na orodha ya watu maarufu ambao wameshinda tuzo ya ubalozi wa watu walio na dhamira ya kubadilisha uovu katika jamii, akiwemo rais wa kwanza Afrika kusini Nelson Mandela na msanii wa China Ai Weiwei.

Msomaji wa makala haya itakuwa vyema kuufahamu wasifu wa mwanamama huyo Angelique Kidjo. 

Yeye ni mwanamuziki mashuhuri aliyejizolea sifa lukuki katika umahiri wa kutunga na kuimba nyimbo zenye maudhui yanayokubalika katika jamii.

Anafahamika sana kwa mtindo wake wa kuchanganya miondoko mbalimbali ya kimuziki ya Afro pop, Afro beat, reggae, muziki wa dunia, Jazz, muziki wa injili na Latin.

Kidjo katika usifu wake unaeleza kuwa ni mtu mzima kwa umri ambae Julai 14, 2016 atatimiza miaka 56 tangu azaliwe Julai 14, 1960 katika mji wa Ouidah huko Jamhuri ya Benin, Afrika ya Magharibi.

Kwa wale wanaojuwa Jiografia vizuri watabaini kuwa nchi hiyo zamani ilikuwa ikiitwa Dahomey. 

Hadi sasa anaendeleza talanta zake za utunzi na uimbaji wa muziki wa Afropop, Afrobeat, Reggae, muziki wa dunia, Jazz, muziki wa Injili na Latini. 

Wakati akiwa na umri wa miaka sita, Kidjo alianza kijihusisha na kikundi cha Kibisa kilichokuwa kinamilikiwa na mama yake mzazi. Mama huyo ndiye akawa anampa kipaumbele sana katika muziki na kucheza pia.

Lakini kuendelea kwa machafuko ya kisiasa nchini Benin, kulipelekea Kidjo kukimbilia katika jiji la Paris nchini Ufaransa, mnamo miaka ya 1982.

Mwaka huo huo ndipo mkongwe huyo alipoianza kazi ya  muziki mpaka hivi sasa bado anaendeleza talanta yake.

Alianza kama mwimbaji wa bendi za vichochoroni kabla ya kuanzisha bendi yake mwenyewe, na mwishoni mwa miaka ya 1980.

Kidjo akatokea kuwa mmoja kati waimbaji maarufu wa jukwaani huko Paris na amewahi kushinda mara tano tuzo ya Grammy kama mtunzi na mwimbaji bora. 

Aidha Angelique pia talanta ya ubunifu mzuri wa ‘sini’ za video.

Kidjo ni mama wa familiya ya mume ambaye pia ni mwanamuziki na mtayarishaji aitwae Jean Hebrail.
Wamebahatika kupata mtoto mmoja aitwae Naïma, aliyezaliwa mwaka 1993.

Kama walivyo wanamuziki wengi wenye mafanikio mazuri, Kidjo kwa sasa anaishi New York, huko Marekani akifanya shughuli za muziki na zinginezo.

Nguli huyo amekuwa balozi wa kujitolea wa Shirika la Umoja wa Mataifa la UNICEF tangu 2002.

Kidjo katika juhudi zake za maendeleo zilipelekea kuanzisha mfuko uitwao Batonga Foundation. Mfuko ambao una lengo kubwa la kutoa elimu ya juu ya sekondari kwa wasichana kwa madhumuni ya kuwapa mwongozo wa maisha katika kuibadilisha Afrika. 

Batonga Foundation pia unakubali ufadhili wa wanafunzi, kujenga shule za sekondari, kuongeza uhandikishaji zaidi, kuboresha viwango vya ufundishaji, na kukimu uenezaji wa shule. 

Adha mfuko huo husaidia mipango endelevu katika elimu, kutafuta njia ya mbadala ya elimu na kiuwakilisha katika jumuiya kuwa kama ndio kutambua thamani ya elimu kwa wasichana.

Angelique Kidjo aliwahi kutamba kwa wimbo uliomuongezea umaarufu ni wa ‘Agollo’.

Katika video ya wimbo huo anaonekana akitamba jukwaani huku akiwa kanyoa kiparakichwani.

Mwanamama huyo amekwisha fyatua albamu nyingi zikiwemo za ‘Parakou’ aliitoa mwaka 1990, ‘Longozo’ ya 1991, ‘Aye’ ilitoka mwaka 1994 , ‘Fifa’ ya mwaka 1996 na ‘Oremi’ ya mwaka 1998.

Alipiga nyimbo mchanganyiko zikiwemo za Black Ivory Soul ya mwaka 2002, Oyaya ya mwaka 2004 na Djin Djini ya 2007.

Aidha Kidjo aliwahi urekodi nyimbo nyingi tu kwa ajili ya filamu mbalimbali.

Amekwisha tunukiwa tuzo zikiwemo za Octave RFI na Prix Afrique en Creation alizopokea mwaka 1992. 

Kidjo pia aliwahi kurekodi nyimbo nyingi kwa ajili ya filamu mbalimbali.

Alipata tuzo ya uimbaji bora wa kike mwaka 1995, kwenye  Kora Music Awards, mwimbaji bora kike wa Afrika mwaka 1997 na tuzo ya Mobo ya mwaka 2002.

Grammy ilimtunuku tuzo kupitia kipengele cha nyimbo bora ya Video ya mwaka 1995 na albamu bora ya Dunia kwa mwaka wa 1999, 2003 na 2005. 

Mwisho.






No comments: