Monday, September 7, 2015

MZEE WA FARASI ALLY CHOKI.




 MZEE WA FARASI ALLY CHOKI.
Ally Choki ni mwanamuziki anayetamba miongoni mwa wanamuziki wa muziki wa dansi hapa nchini.
Ana talanta vingi zilizojengeka kichwani mwake zikiwemo za kutunga, kuimba pamoja na uongozi.
Historia yake katika muziki Choki iliieleza kwamba alianza muziki rasmi mwaka 1988 nilipojiunga na bendi ya Lola Africa.
Baadae akajiunga na bendi ya Mwenge Jazz iliyokuwa chini ya Jeshi la Wananchi Tanzania(JWTZ).
Hakudumu kwa kipindi  kirefu baada ya miezi sita alihamia katika bendi ya Bantu Group iliyokuwa ikiongozwa na ‘Komandoo’ Hamza Kalala.
“Mwaka 1990 nikiwa Bantu na Hamza Kalala akiwa kiongozi tulitoa albamu ya Baba Jane. Mwaka 1991 nilitoka Bantu, nikajiunga na Legho Stars chini ya Tshimanga Kalala Asosa...” alisema Ally Choki
Safari ya kusaka mafanikio ilikuwa ikisababisha kwenda huku na kule. Alijikuta yuko katika bendi ya Legho Stars. Hata hivyo huko nako hakudumu sana akaamua kurudi katika bendi ya Bantu group.
Choki alikuwa mithiri ya 'Kunguru' kwani  huko Bantu group nako hakukaa sana, akaenda kujiunga na  bendi ya Bendi ya MK Beat ‘Tukunyema’, iliyokuwa ikiongozwa na Shem Ibrahim Karenga.
Mwaka 1992 alihamia katika bendi ya Washirika Stars ‘Watunjatanjata’ ambako walitoa albamu iliyopewa jina la Gubu la Wifi. 
Huko aliwakuta mwimbaji mwingine mahiri akiwemo Adam Bakari ‘Sauti ya Zege’, mpapasaji Kinanda Abdul Salvado ‘Father Kidevu’ na wengine wengi.

Katika harakati za kusaka maisha Choki aliamua kuvuka mpaka wa nchi nakuingia  katika jiji la Nairobi, nchini Kenya mwaka 1994.
Akiwa katika jiji hilo aliungana na wanamuziki wengine akiwemo Muumini Mwinjuma, ambako huko wakaanzisha bendi yao ikiitwa 'Extra Kimwa' mwaka 1998.
Choki ilipotimu mwaka  mwaka 1999, aliamua kurejea nchini  baada ya kupata taarifa kuwa mama yake mzazi kuwa alikuwa mgonjwa.
Akiwa hapa nchini aliamua kujiunga katika bendi ya The African Stars ‘Twanga Pepeta’  chini ya uongozi wa mkurugenzi Asha Baraka. 
 Alikubali kujiunga na bendi  hiyo baada ya kupokea ushauri kwa mwanamuziki mwenzake Robert Hegga ‘Caterpillar’ ambaye walikuwa wote Nairobi.
Mwaka 2000 walitoa albamu iitwayo 'Jirani', iliyokuwa na nyimbo nyingi lakini hiyo ulikuwa ni utunzi wake yeye Choki.

Kama kuna kitu ambacho hawezi kukisahau wakati akiwa Twanga, ni pale wanamuziki wengi waliihama bendi hiyo na kwenda kujiunga na bendi nyingine ya Chuchu Sound. Baadhi yao wakatimkia katika bendi ya Mchinga Sound, akiwemo Adolf Mbinga aliyekuwa gitaa la mpiga solo.
Busara zake akazitumia kwa kumfuata mpiga solo mwingine Miraji Shakashia ‘Shaka Zulu’.
Shakashia naye hakudumu kwa kipindi kirefu akatimka ndipo nafasi yake ilishikwa na Kassim Rashid ‘Kizunga’ aliyekuja kupiga gitaa la rhythm.
Baadaye alipewa cheo kuwa kiongozi wa bendi na ndipo walipotengeneza albamu ya Fainali uzeeni. Albamu hiyo ilifuatiwa na ile ya ‘Ukubwa Jiwe’ hatimae ‘Chuki Binafsi’.
Ally Choki alikuwa na kila sababu  za kujivunia akiwa hapo Twanga, kwa kuwa alikuwa akiongoza kwa kutunga nyimbo nyingi zilizovuma.
Baada ya kujipima uwezo wake, akanzisha bendi yake ya Extra Bongo mwaka 2003. Bendi hiyo ilikusanya wanamuziki wengi mahiri hapa nchini na kuweza kuwa tishio kwa bendi zingine hususan katika jiji la Dar es Salaam.
Lakini kama wasemavyo waswahili “Penye riziki hapakosi fitina” ndivyo ilivyotokea kwa Ally Choki ambapo fitina ikatengenezwa  na wanamuziki wake wakanunuliwa akabaki ‘mweupe’ pasipo na mwanamuziki.
Kutokana na hali hiyo, alilazimika kuiacha bendi yake na kwenda kujiunga katika bendi ya Mchinga.
Huko nako hakudumu kwa kipindi kirefu, akarejea tena Twanga Pepeta. Baadae tena akajiunga na kundi zima la Tanzania One Theater, lililokuwa likiongozwa na Kapteni mstaafu John Komba.
Akiwa ni mmoja wa viongozi wa TOT, Choki alifanikiwa kuipandisha chati bendi hiyo baada ya kuwaleta wanamuziki toka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Alidumu na bendi hiyo ya TOT hadi mkataba wake  ulipokwisha, akaamua kuifufua tea bendi yake ya Extra Bongo mwaka 2009.
Ally Choki akizungumzia kisa cha sababu za kushuka kwa kiwango cha muziki wa dansi, Choki alikanusha kauli hiy.
Alisema kwamba muziki wa dansi haujashuka kiwango isipokuwa vyombo vya habari vimeupa kisogo kwa kuangalia zaidi muziki wa Bongo Fleva licha ya wao kuntoa nyimbo nzuri na hata video nzuri.

“Uongozi wa bendi za muziki ni mgumu ukilinganisha na mwanamuziki wa Bongo Fleva ambapo kiongozi hana wanamuziki wengi. Hata hivyo naamini ni wakati na kuna muda utafika muziki huu utakuwa juu…” alisema Ally Choki.
Choki akithamini mchango mkubwa wa wanamuziki waliomtangulia, alimuelezea marehemu Muhidin Maalim Gurumo kuwa alikuwa mwalimu na mtu anayesikiliza ushauri.
Alisema kwamba yeye binafsi nilifanya naye kazi nyingi zikiwapo zili waizotoa albamu yenye nyimbo zake tatu na za Gurumo tatu.
“Album hiyo ilifanya vizuri sana na tulipata fedha nyingi mpaka kila ninapokutana naye akawa anasema nakushukuru sana kijana….” Alisema Ally Choki.
Akielezea siri ya mafanikio yake , Choki alieleza kuwa yanatokana na yeye kufanya juhudi, kutokunywa pombe aliyoanchana nayo mwaka 1994.
Aidha amesema kwamba havuti sigara, amefanikiwa kujenga nyumba,kununua gari aidha ni baba wa familiya ya mke na watoto sita.

Ikumbukwe kabla ya kuondoka The African Star, Choki alikwaruzana na mkurugenzi wa ASET Asha Baraka. Katika  purukushani hizo alifika mbali kwa kutoa kiapo kibaya dhidi ya Mkurugenzi wake Asha Baraka.

Choki akasema kitendo cha ASET kumpeleka mahakamani kumdai gari ambalo walimpa mwenyewe kilimkera sana. Pia ASET kukataa kurudisha pesa za Miraji Shakashia vilevile ASET kutothamini michango ya wasanii walioizalishia ASET pesa nyingi.

Msomaji wa makala haya hauwezi kaumini kwamba Choki hivi karibuni amerejea tena kwa kishindo kwenye bendi yake ya zamani ya African Star Entertainment (Twanga Pepeta)
Alitanganzwa mbele ya waandishi wa habari na Mkurugenzi wa ASET, Asha Baraka aliyekuwa amefuatana na Katibu wa bendi, Luiza Mbutu.
Mwisho.






No comments: