Sunday, November 1, 2015

MJUE "JIM REEVES" ALIYETAMBA KATIKA ULIMWENGU WA MUZIKI


MJUE "JIM REEVES" ALIYETAMBA KATIKA ULIMWENGU WA MUZIKI

Hapana shaka watu wazima wenye umri wa mkubwa kama wangu, ukitamka jina la Jim Reeves, unakuwa umewakuna vilivyo.

Alikuwa ni mwanamuziki wa Kimarekani aliyejikita katika miondoko ya muziki wa ‘Country’ na muziki wa kawaida kama  mtunzi haklikadhalika uimbaji.

Reeves aliweza kuweka rekodi ya muziki wake ukupanda chati toka miaka ya 1950 hadi ya 1980.   

Muziki wake ukawa maarufu na kujulikana kama mwanamuziki wa midundo ya ‘Nashville’ (ambayo ni mchanganyiko wa muziki wa zamani wa country na ule wa kisasa). 

Wasifu wa nguli huyo unaonesha kuwa  jina lake halisi alikuwa ikiitwa
James Travis aka “Jim” Reeves aliyezaliwa Agosti 20, 1923 Reeves amezaliwa katika kitongoji cha Galloways huko Texas, nchini Marekani.

Alitambulika kama ‘Muungwana Jim’ na nyimbo zake ziliendelea kupanda chati kwa miaka kadhaa hata baada ya kifo chake.
Reeve alikuwa akitoka katika jamii ya watu waliokuwa nje ya mji karibu na Carthage. Alifariki Julai 31, 1964 akiwa na umri mdogo wa miaka 40 katika ajali ya ndege binafsi.

Yeye alikuwa mwanachama wa muziki wa ‘Country’ na pia ule wa Texas Country Halls of Fame.

Jim alifanikiwa kupata nafasi ya kusomamsomo ya juu ‘Scholarship’ ambapo alijisaljili kusomea masuala ya kuhutubia na maigizo.

Baada ya miezi sita katika masomo hayo, aliachana nayo akaamua kwenda kufanya kazi katika yadi ya kutengeneza Meli huko Houston.

Licha ya kuwa na weledi katika muziki Reeves pia alikuwa mwanariadha aliyewahi kuchezea ligi za Semi-Professional kabla hajaingia mkataba na St. Louis Cardinals, timu ya shamba. Mwaka 1944 alicheza kama right-handed Pitcher. 

Aidha alicheza ligi ndogo kwa miaka mitatu kabla hajaumia na kupata maumivu katika misuli iliyohitimisha juhudi zake za kuendelea na michezo.
Reeves alianzia kufanya kazi kama mtangazaji wa radio. 

Kila wimbo umalizikapo kuupiga radioni, yeye akawa anaimba wimbo huo.

Mwishoni mwa miaka ya 1940, aliingia mikataba na baadhi ya Makampuni madogo ya kurekodi, huko Texas lakini hakupata mafanikio. 

Muziki wa Magharibi ulimfanya kuhamasika sana hususani alipokuwa akiwasikia wanamuziki kama Jimmie Rodgers na Moon Mullicann. 

Waimbaji wengine maarufu wakati huo aliokuwa akiwatamani ni akina Bing Crosby, Eddy Arnold na Frank Sinatra.

Mapenzi hayo makubwa katika muziki yalimpelekea kuwa mwanachama wa bendi ya Moon Mulican.

Jim aliweza kufanya mitindo ya mwanzoni za bendi ya Mullican, nyimbo zake kama ‘Each Beat of My Heart’ na ‘My Heart’s Like a Welcome Mat’ mnamo miaka ya 1940 mwishoni na mwanzoni 1950.
 
Reeves aliweza kuimba nyimbo za ‘Mexican Joe’ ambazo zilishika namba moja mwaka 1953.

Kutoka mwaka 1955 mpaka kuendelea mwaka 1969 Reeves nyimbo zake ziliendelea kushika ‘ukanda’ hata baada ya yeye kufariki.

Nyimbo zake za kwanza za ‘Country’ zilizompa mafanikio zilikuwa ni pamoja na ‘I Love You’ alouimba akishirikiana na Ginny Wright, na ‘Mexican Joe’ ‘Bimbo’.
 
Nyimbo nyingine zilizotolewa na Fabor Records na Abbott Records ilitoa albam yake ya kwanza Novemba, 1955 iliyojulikana ‘Jim Reeves Sings’. 

Mapema mwaka 1955, Reeves alisaini mkataba wa miaka 10 na Kampuni ya RCA Victor chini ya Steve Sholes, ambaye alitoa rekodi za kwanza za Reeves akitumia Kampuni ya RCA na pia akaingia mkataba na Elvis Presley na kampuni hiyo hiyo mwaka huo huo.

Alipokuwa akirekodi mwanzoni akiwa na  Kampuni ya RCA, Reeves bado alikuwa anaimba kwa staili ya sauti ya juu ambapo ilionekana ndio kipimo cha nyimbo za ‘Country’ Wanamuziki wa Magharibi kwa wakati huo. 

Baadaye Jim alianza kupunguza sauti yake wakati akiimba na kutumia ‘Pitch’ ya chini akiimba huku midomo yake ikikaribia kugusa kipaza sauti, ingawaje waliokuwa wanamrekodi (RCA) walikuwa wanailalamikia hali hiyo. 

Mwaka 1957 kwa maelekezo ya ‘Produysa’ wake Chet Arkins alitumia mtindo huo katika toleo la wimbo wa maonesho wa ‘Penzi lililopotea’ uliokusudiwa uimbwe na mwimbaji wa kike.

Katika kipindi chote miaka yote ya 1950 na hadi 1960 mwanzoni, Jim Reeves aliachia nyimbo zake kali zizoshika ‘chati’ za ‘Anna Marie’ na  ‘Blue Boy’ No. 2 za mwaka  1958.

 Alifyatua kibao kingine cha ‘Billy Bayo’ mwaka 1959 na  ‘He will have to go’ wa mwaka 1960., ‘Adious Amigo’ (namba mbili, 1962), ‘Welcome to my World’ (namba mbili, 1964) na ‘I guess I’m crazy’ (namba moja kwa wiki saba, 1964).
Jim Reeves  pia alikuwa na kikosi na idara ya nyimbo za dini katika jukwaa lake.
Wimbo wake, ‘Danny Boy’ akijitambulisha kwamba wazazi wake wametokea Irish. Wimbo ‘But You Love Me Daddy’ ukirekodiwa wakati mmoja akiwepo ‘Steve’ mtoto wa miaka minane wa mpiga gitaa la besi, Bob Moore, ulikuwa katika ishirini bora huko Ulaya miaka kumi Baadaye. 

Rekodi zake mara nyingi zilikuwa na utamanifu wa kipekee, kama ‘I Love you Because’ (ulishika namba 5) na ‘I won’t forget You’ (namba 3) zilikuwa katika chati huko UK kwa wiki 39 na 25 mfululizo.

Reeves alikuwa amesaidia sana kuanzisha staili mpya ya muziki wa ‘Country’ akitumia ‘violin’ na ‘mpangilio wa kupendeza wa background ikijulikana kama ‘Nashville’ sound.   

Alipata umaarufu kama muimbaji wa kiume mwenye sauti ya kupendeza na nzito kiasi, yenye madaha. 

Nyimbo kama ‘Adios Amigo’ ‘Welcome to My World’ na ‘Am I Losing You’ zinaonyesha hili. 

Nyimbo zake za Chrismas zikijirudia rudia na kupendwa sana hasa zikiwa ni pamoja na ‘Chrismas’ ‘Blue Chrismas’ na ‘An Old Chrismas Card’.
 
Hali kadhalika Jim Reeves amekuwa hodari kwa kuukweza na kuzipa maarufu nyimbo nyingi za ‘Injili’ kama ‘We Thank Thee’ ‘Take My Hand, Precious Lord’ ‘Across The Bridge’ ‘Where We’ll Never Grow Old’ na nyingine nyingi.

Reeves aliibua mafanikio makubwa kwa utunzi wa Joe Allison, ‘He’ll have to Go’. 

Kwa kweli kulikuwa na mafanikio makubwa kwa muziki huu wa kawaida na wa ‘Country’ ambapo ulimpatia ‘Platinum Record’ ambayo ilitolewa mwishoni mwa mwaka 1959 na ilifanikiwa  kuwa namba moja katika gazeti la ‘Billboard’. 

Katika nyimbo za ‘Country’ ambazo zili ‘hit’  kuanzia 08/February, 1960 na kuendelea kwenye chati kwa wiki 14 mfululizo hii moja wapo.

Mwana historia wa muziki wa Country, Bill Malone alionesha kwamba ni katika namna nyingi Reeves aliendeleza utamu na ubora katika   muziki wa ‘Country’ kimpangilio na ‘melodi’ safi na ujumbe unaogusa  mioyo ya watu. 

Kwa nyongeza, Malone alimsifia Reeves kwa staili yake ya kuimba ambayo anaishusha chini sauti yake, inakuwa kama ya kubembeleza na ndio maana watu wengi wanatamka kwamba Jim Reeves ni muimbaji mwenye sauti ya mguso.

July 31, 1964, Reeves na mshirika mwenzake wa kibiashara, Meneja Dean Manuel waliondoka Batesville, Arkansas kupitia Nashville wakitumia ndege ya injini moja akiwa Reeves anaendesha.

Wawili hao walikuwa wamepata ‘dili’ ya kununua shamba huko Deadwood Texas, Kaskazini mwa Galloway ambayo ni sehemu aliyozaliwa Reeves.

Wakati wanapaa juu kwa ndege akiwa na  Brentwood, Tennessee, walikutana na dhoruba ya upepo mkali na mvua kubwa.

Katika uchunguzi ilionekana ndege hiyo ndogo ilinaswa katika dhoruba na Reeves alipata mstuko ikaanguka na wao wakafariki. 

Mjane wa marehemu, Mary Reeves  alianzisha uvumi kwamba Reeves alikuwa akiendesha juu chini na aliongeza spidi ili kukwepa  dhoruba.

Hata hivyo kulingana na Larry Jordan, maelezo ya mjane wake kwamba Reeves alikuwa anaendesha chini juu si sahihi.
Kutokana na watu walioiona ajali hiyo jinsi ndege ilivyoanguka na  maelezo yaliyomo kwenye tape iliyorekodi mwenendo wa ndege.

Pia maelezo ya ripoti ya ajali, kwamba Reeves alikata kushoto katika jitihada zake za kuipata Franklin road ili afike uwanja wa ndege aweze kutua.  

Katika jitihada yake hiyo  akazidi kuelekea kule kwenye mvua kubwa.

Katika kuhangaika ili akakipate kiwanja ili kutua,  spidi ya ndege ikawa ipo chini hivyo akaikwaza ndege. 

Reeves alitegemea zaidi hisia zake katika kumuongoza na hakutumia maarifa  aliyofundishwa chuoni kuikabili hali kama hiyo. 

Baada ya masaa 42 mabaki ya ndege yalionekana ikiwa  mbele, yaani usoni pamoja na injini vimejikita ardhini.  Reeves na mwenzake walikutwa tayari wamekwisha fariki.

Jim Reeves alizikwa katika kipande cha ardhi maalum ubavuni mwa ‘Highway 79’ Texas.

Licha ya kufariki Jim Reeves bado umaarufu wake haukupotea, kwa hakika mauzo ya kazi zake yameongezeka baada ya kufariki.
  
Mjane wake, Mary Reeves (70) alifariki katika siku ya ‘Veteran’ Tarehe Novemba 11, 1999, iliripotiwa kuwa amekufa akiwa peke yake katika nyumba ya kuuguza wagonjwa. 

Hata hivyo mazishi yake yalipangwa kwa watu wachache tu wa karibu ikiwa hii ni agizo la aliyekuwa mumewe wa pili Tery Davis.

Tangu kipindi cha kifo cha Jim Reeves kulipotokea, Mary alipatwa na matatizo ya kuugua kabla hayajamzidia. 

Alikuwa ni kiungo muhimu katika kuuweka muziki wa Reeves na kumbukumbu zake alizifanya kuwa hai.

Kutokana na Mary Reeves Davis kushindwa kutokana na ugonjwa kuzisimamia mali za Jim Reeves ziliuzwa kwa ‘United Show of America’ mwaka 1997 kwa thamani  ya Dola za Kimarekani milioni 7.3
Jim Reeves aliwekwa kwenye kundi la mwimbaji Nyota wa Kiume ambaye ametokeza katika midundo ya ‘Nashville Sound’.
Sauti yake laini ya kidume yenye madaha imeendelea kusikika hadi wakati leo.

Mwisho.


No comments: