Friday, October 14, 2011

Eddy Sheggy akikuletea Shakaza 'live'

Jambo ambalo naliona wazi ni kuwa Watanzania wanapenda sana nyimbo za dansi zinazotokana na nyimbo zenye asili ya makabila ya hapa Tanzania. Nikikumbuka nyimbo kama  Mtaulage, Malaine, Nyongise, ambazo ni kazi yangu mwenyewe nikiwa Tancut na Vijana Jazz, kila Munu ave na kwao ya Les Mwenge, Boko wa Kilimanjaro Band, Shakaza ya Bantu  na nyingi nyingine zote zilichukua nafasi ya juu katika anga za muziki wakati wake, na hata sasa. Pengine lingekuwa somo kwa wanamuziki wa Tanzania na kuliangalia hili katika tungo zao. Hebu tumkumbuke Eddy Sheggy hapa akiwa na Bantu, akiimba na ndugu zaki Francis na Christian

No comments: