Monday, April 14, 2014

BOZI BOZIANA ' MZEE BENZI'



BOZI BOZIANA NA ANTI-CHOC



Aprill 15,2014.

Bozi Boziana au ‘Mzee Benzi’ kama anavyojulikana na wengi ni mwanamuziki anayeongoza kundi zima la Anti Choc toka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.
Jina lake kamili anaitwa Mbenzu Ngamboni Boskill ambaye alizaliwa  mwaka 1952 huko Jamhuri ya Kidemkokrasia ya Kongo.
Pamoja na utunzi na uimbaji Bozi pia ni mkung’utaji mzuri wa gita aliyepiga katika bendi nyingi kubwa nchini mwao zinazopiga katika mtindo wa soukous.
Baadaye akaunda bendi yake Orchestra Anti-Choc.
Mzee Benzi aliazia muziki wa Afro-Pop katika  bendi ya Air Marine lakini alianza kuyaona mafanikio ya kazi zake ilipotimu mwaka 1974 alipojiunga na bendi ya Zaiko Langa Langa. Zaiko LangaLanga ilikuwa na waimbaji  mashuhuri wakati huo  wakiongozwa na mkongwe  Papa Wemba na mwezake Evoloko Jocker.
Lakini haikuzidi mwaka , Papa Wemba na Evoloko waliondoka Zaiko Langa Langa na Bozi Boziana aliwafuata  kwenda kuanzisha bendi mpya ikaitwa Isifi Lokole.
Kutokukubaliana katika maswala mbalimbali ya msingi kulimfanya wanamuziki Papa Wemba, Boziana, Mavuela Somo na wengine kuondoka bendi ya Isifi Lokole na wakaunda bendi mpya iliyopewa jina la Yoka Lokole.
Yoka Lokole ilipata  mafanikio makubwa mwaka 1976  lakini mwinshoni mwa mwaka huohuo Papa Wemba aliicha bendi hiyo na akaenda kuanzisha bendi ya Viva la Musica.
Bozi Boziana naye mwaka 1977 akaondoka Yoka Lokole licha ya bendi hiyo kuwa maarufu kwa kipindi kifupi.
Kwa miezi michache  Boziana alishirikiana na mwanamuziki Efonge Gina, ambaye naye alikuwa katika bendi ya Zaiko Langa Langa. Walirekodi nyimbo kadhaa kama vile Selemani iliyotungwa na Bozi na  Libanko Ya Ngai utunzi wake Gina.
Produza  Verckys Kiamuangana mwaka 1981  aliibadilisha  bendi ya Soukous super group  na kuita  Langa Langa Stars ikiwa imesheheni vipaji vya wanamuziki kaiwemo Evoloko Jocker, Dindo Yogo na  wnengine wengi.  Bozi Biziana aliakwa kujiunga vijana hao naye akaubali na kuicha  Zaiko Langa kwa mara ya pili.
 Langa Langa Stars ilidumu kwa miaka michache iliyofuatia kabla na Boziana naye akaondoka kwenda kujiunga na bendi kubwa nchini humo  Choc Stars aliyokuwa chini Ben Nyamabo ambako alipiga hadi mwezi Novemba 1985.
Akiwa na bendi hiyo ya Choc Stars Boziana alirekodi baadhi ya nyimbo ambazo zilikuja kuwa maarufu za Sandu Kotti, Alena, Mbuta-Mutu na Retrouvailles a Paris.
Anti –Choc ilikuwa na wanamuziki wengi wenye vipaji lukuki wakiwemo akina Fifi Mofude, Djo Nolo, Koffi Alibaba, Wally Ngonda, Rigo Star, Ngouma Lokito, Deesse Mukangi, Marthe Lamugenia, Ngimbi Yespe na Maoussi Solange.
Mpiga gita wa kwanza katika bendi hiyo alikuwa Matou Samuel ambaye  kwa sasa anaimba muziki wa Injili  na nafasi yake ilishikwa na Dodoly ambaye kabla ya kujiunga humo alitokea katika bendi ya mwanamuziki Lita Bembo ya Orchestre Stukas.
Dodoly alipachikwa jina bandia la ‘The sewing machine’ kwa umahiri wake wa kutumia vidole vyake kucharaza nyuzi  kwa kasi kubwa.
Tokea miaka ya 1980  Boziana aliendelea katika bendi yake ya Anti-Choc ikiwa ni pamoja na kurekodi nyimbo  akishirikiana na wanamuziki wengine mahiri.
Boziana aliwahi kushinda zawadi ya Kora All-African kwa album yake kuwa bora toka nchi za Afrika ya Kati.
Kwa wapenzi wa muziki hapa nchini watamkumbuka Bozi jinsi alivyoteka wapenzi katika maonesho kadhaa aliyoyafanya hapa nchini kwa ushirikiano walioonshea kati ya Bozi Boziana, Deesse Mukangi na Joly Detta walivyokuwa wakilishambulia jukwaa kwka staili ya ‘Nzawisa’ katika nyimbo za Tembe na Tembe, Palpitation na zingine nyingi zilifanya watu kuviacha viti vyao kwenda kuwatuza.
Bozi Boziana ana sauti nzuri, yakupendeza akimba huku akipokezana na timu yake ya wanadada wawili, Joly pamoja na Deesse.
Sifa nyingine za mwanamuziki huyu mzee Benzi ni kwamba muziki wake hauna mwingiliano kati ya sauti ,gitaa na synthesizer katika nyimbo zake zote. Mfano katika wimbo wa ‘Ngoyartong020’ tune tatu za mwanzo Boziboziana amemshirkisha Jolly Detta na Deesse,  na sehemu ya pili ya wimbo huo aliongeza nguvu kwa kumuongeza waimbaji na wanenguaji  Scola Miel maarufu kwa jina ‘Nzawissa’ na Betty. Bozi alifyatua vibao vingi vilivyompa sifa nyingi ukiwemo wa La reine de Sabah, Lelo Makambo Lobi Makambo Evelyne na Fleur de Lys ambazo alimshirikisha mwimbaji wa kike Joly Delta.
Boziana aliachia wimbo mwingine akimshirikisha Deesse na Ba Bokilo.
Bozi Boziana na bendi yake bado anaendeleza muziki akiwa na bendi yake na watanzania watakumbuka kwa mara ya mwisho alikuja hapa nchini kwa mwaliko wa African Stars Entertainment Tanzania (ASET) iliyo chini ya uongozi wa Mkurugenzi Asha Baraka.

Mwisho.


No comments: