Saturday, April 16, 2016

MTUNZI NA MWIMBAJI KASONGO WA KANEMA



MTUNZI NA MWIMBAJI KASONGO WA KANEMA
“Kakolele mama Kakolele Kako mama Kako mama…Viva Krismasi… Viva Krismasi, Viva mamaa…, Noele Mamaa…Noele mamaa.. ” 

Haya ni maneno yanayosikika katika wimbo wa Viva Krismasi ambao bado siku chache yataanza kusikika tena katika vituo vya redio humu nchini na Afrika Mashariki kwa ujumla kukaribisha sherehe za Krismasi na Mwaka mpya wa 2016.

Matamshi ya maneno hayo hutamkwa mwimbaji Kasongo wa Kanema wakati alipokuwa katika bendi ya Baba Nationale iliyokuwa ikiogozwa na Baba Gaston Ilunga wa Ilunga. 

Bendi hiyo ilikuwa na makao makuu yake katika jiji la Nairobi nchini Kenya.

Katika makala haya yatamzungumzia mwanamuziki huyo Kasongo wa Kanema, aliyekuwa na vipaji  vya utunzi na mwimbaji wa muziki wa dansi.

Ni mwenye asili toka Jakhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), aliyeanza muziki  akiwa na umri mdogo wa miaka 10 huko nchini mwake.

Kasongo wakati akijifunza kuimba, alikuwa akitamani kufikia viwango vya nguli wa muziki za Franco Luambo Makidi na Tabu Ley. Hivyo alichukua muda mwingi kusikiliza nyimbo zao pia kuziimba.

Familiya yake haikumtupa, ilimpa moyo baada ya kumuona kuwa ana juhudi za kuupenda muziki. 



Akiwa na  wenzake waliokuwa na mawazo kama yake, walifikia kuunda bedi ya Super Mazembe.
Wanzake hao walikuwa akina Atia Joe, Lovi Longomba, Bukalos Kayembe Rapok, Songole, Lobe Mapako, Talos, Longwa Didos nan Fataki Lokasa Losi Losi ‘Masumbuko ya duniya’,  hawa wote walikwisha tangulia mbele za haki. Kati yao walio hai yeye Kasongo wa Kanema na anayeishi katika jiji la Nairobi na  Dodo Dorris, ambaye anakula maisha huko Afrika ya Kusini.

Wanamuziki wengine walikuwa wakiunda kikosi cha Super Mazembe ni pamoja na Kasongo Songo  au maarufu kama Kasongo Jnr. 


Huyo alikuwa akipapasa kinada  na kuimbaj. Aidha alikuwepo Maranata, gitaa zito la besi liliungurumishwa na Kashindi , kwenye gitaa la solo alikuwa Alpha Nyuki na Ale Maindu. 

Mcharanga drums alikuwa Lei Mkonkole na Longwa Disco alikuwa mwimbaji.

Kasongo  anaishi katika jiji la Nairobi ni baba wa familiya ya mke  aitwaye Achieng, na wamebarikiwa kupata watoto watano.

 
Mwisho.


No comments: