Saturday, April 16, 2016

WAMKUMBUKA MKONGWE JIMMY MONIMAMBO?



WAMKUMBUKA MKONGWE JIMMY MONIMAMBO?
Wapenzi wa muziki wa dansi hapa nchini wanatakumbuka wimbo wa Sisili ulioimbwa kwa umahiri mkubwa na bendi ya Orchestra Shika Shika.
Ilikuwa ikiongozwa na mwanamuziki Jimmy ikiwa na  makao makuu yake katika jiji la Nairobi, nchini Kenya.
Shika Shika ilikuwa ikichuwana vikali na bendi zingine kubwa zikiwemo za Super Mazembe, Les Mangelepa, Baba Gaston, Les Wanyika na nyingine nyingi.
Akiwa na bendi hiyo ya Shika Shika walitoa album yao ya kwanza mwaka 1982, iliyotikisa jiji la Nairobi na mbili zaidi alizitoa mwaka uliofuatia.
Katika safu ya waimbaji alikuwepo Lovy Longomba ambae alitunga wimbo wa Tika Nalela, ulioibeba kwa kaisi kikubwa Shika Shika  na yingine zikiwemo za  "Sisili," "Amba," na "Inyo"
Wasifu wa Jimmy Monimambo anaeleza kuwa alizaliwa katika jiji la Kinshasa, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
Wazazi wake wake walikuwa raia wa  Angola, waliokuwa miongoni mwa raia walioikimbia nchi yao ya Angola na kwenda kuishi nchini Kongo wakitafuta kazi.
Monimambo pia alifahamika kwa majina ya Jimmy Monimambo Mfumu Ntoto “Mfalme wa dunia”, aliyewahi kupiga muziki katika bendi ya Ochestra Maquis du Zaire, ilikuwa na makao yake makuu katika ukumbiwa wa White House , maeneo ya Ubungo jijini Dar es Salaam.
Baadae akajiunga katika bendi ya Orchestra  Shika Shika, pia alikwenda kujiunga katika bendi za  Special Liwanza, Boma Liwanza, na Viva Makale iliyokuwa ikiongozwa na Kalombo Mwanza George.
Baadhi ya wanamuziki waliounda Shika Shika walikuwa Jimmy Monimambo  Vicky Longomba "Lovy" na Moreno Batamba, aliyekuwa mwimbaji mwenye sauti nzito yenye mvuto. Wengine walikuwa ni pamoja na Bwami Walumona  na Kasongo Kanema.
Wengi wa wanamuziki hao kabla ya kujiunga katika bendi ya Orchestra Shika Shika walikuwa katika bendi ya Baba Gaston Nationale, iliyokuwa ikiongozwa na  Baba Gaston Ilunga wa Ilunga.
Safu hiyo ilinogeshwa zaidi na wanamuziki akina Lawi Somona, Sammy Mansita, mpiga gitaa Mwalimu Siama Matuzungidi, na aliyekuwa mcharanga  drums Lava Machine.
Hao kwa pamoja walitoka katika bendi ya Virunga iliyokuwa ikiongozwa na Samba Mapangala.
Safari ya mwanamuziki Monimambo ilimfikisha kuungana na Lovy Longomba kurekodi nyimbo katika studio iliyokuwa ikimilikiwa na bendi za Orchestra Mos Mos na Orchestra Pole Pole.
Safu ya wanamziki waliiuda bendi ya Shika Shika ilikuwa ni waimbaji Jimmy Monimambo, Dago Mayombe na Lovy Longomba wakati kwa upande wa wapiga magitaa walikuwepo Siama Matuzungidi, aliyekuwa akiliungurumisha gitaa zito la besi, aliwahi kupigia katika beni ya Cavacha katika jiji la Kinshasa mnamo miaka ya 1970.

Chery Matumona,Tabu Frantal, Manitcho na kwenye besi alikuwa Silu Waba Nsilu.
Mpiga gitaa Chery Matumona  ambae baadae aliiacha bendi hiyo mwaka 1981, akaenda nchini Uganda na baadae Zambia. Hivi sasa anaishi nchini Canada.
Bendi yake Cavacha iliundwa na waimbaji  Dona Mobeti na Mopero wa Maloba. Mopero baadae aliicha bendi hiyo na kwenda kuunda kundi lake akalipa jina la Orchestra Cavacha de Mopero, ambayo nayo iliingia katika migogoro.
Hatimae nguli wa muziki huo huko DRC Franco Luambo Makiadi, aliingilia kati na kumshawishi Mopero kubuni jina jipya.
Binti ailiyekuwa akiitwa Vicky Shama Shama alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na Mopero wa Maloba, ambae aliamua jia la binti huyo liwe jina la bendi hiyo ikaitwa Orchestra Shama Shama.
Shama Shama iliundwa ikiwa na wanachama toka bendi ya Cavacha, ambayo hata Mopero Wa Maloba alikuwa mwimbaji katika bendi hiyo.
Bendi hiyo ya Shama Shama, alikuja kugawanyika muda mfupi kabla ya safari yao ya kwenda nchini U Uganda.
Hapo ndipo busara za Mopero zilionekana baada ya kusajili wanamuziki wengine wapya aliokwenda na Uganda.
Ule usemi kuwa “La kuvunda halina ubani” ulijionesha wazi pale bendi hiyo ikiwa nchini Uganda  ikasambaratika tena.
Mwanamuziki KoKo Zigo alimshawishi Jimmy Monimambo kuondoka nchini Uganda, wakaunda bendi ya Orchestra Kombe Kombe mwaka 1978 wakiwa na na mwimbaji Koko Zigo. Walifika nchini Kenya wakiwa na bendi hiyo mpya ya Orchestra Kombe Kombe, lakini waliingia mkataba wa kupiga muziki katika ukumbi uliopo Garden Square katika jiji la Nairobi wakiwa wamebadilisha jina la bendi kuwa Orchestra Viva Makale.
Bendi hiyo ilikuwa na wanamuziki mahiri waliokuwa wakitoa burudani maridadi kwa wapenzi wake. Baadhi ya wanamuziki hao ni pamoja na George Kalombo Mwanza aliyekuwa kipuliza saxophone na kuimba, Buami Walumona  na Chery Matumona walikuwa akicharaza gitaa la solo, Siama Matuzungidi, alikuwa akisimama kwa upande wa gitaa la kati la rhythm pamija na Tabu Frantal akiliungurumisha gitaa.
Wengine walikuwa akina Thomy Kabea Lomboto aliyekuwa akiliungurumisha gitaa zito la besi, Coco Zigo, Moreno Batamba, Jimmy Monimambo, Tambwe Mandola wakiwa waimbaji.
Tarumbeta ilikuwa ilipulizwa na Tshamusoke na drums zilicharangwa na Lava Machine.

Jimmy Monimambo alikisha tangulia mbela za haki mungu ailaze roho yake pahala pema peponi, amina.

Mwisho.


No comments: