Sunday, March 10, 2013

GWIJI LA SAXOPHONE DIBANGO LATIMIZA MIAKA 79


GWIJI LA SAXOPHONE  DIBANGO LATIMIZA MIAKA 79 

January 09, 2013

GWIJI LA KUPULIZA SAXOPHONE  MANU DIBANGO  jana Februari 10, 2013 alitimiza miaka 79 ya kuzalikwa kwake. Dibango ni mwanamuziki  aliyejizolea sifa kubwa barani Afrika na ulimwenguni kwa ujumla.

Jina lake halisi ni Emmanuel Dibango ambaye pamoja na kupuliza chombo hicho cha Saxophone, pia ni mtunzi na mwimbaji mahiri mwenye sauti nzito.
Manu Dibango ni kiongozi wa bendi ya Makossa, aliyezaliwa February 10, 1934, katika mji wa Douala nchini Cameroon nchini  Afrika ya Magharibi.
Baba yake alikuwa mfanyakazi serikalini na vilevile alikuwa mtayaarishaji maarufu wa nguo.

Dibango alikuwa mmoja kati ya waanzilishi muziki wa kidunia katika miaka ya 1970. Kwa mantiki  hii ninafahamu vijana wa kizazi cha sasa hawamfahamu ama hawakuwahi kusikia muziki wa nguli huyu. Yawezekana wengi wao walikuwa bado kuzaliwa au walikuwa wadogo nyakati hizo akitamba  Manu Dibango.

Kama kawaida ya wanamuziki walio makini kwa kazi yao, Manu ni miongoni mwao kwani alipiga ‘kitabu’ na kupata elimu yake katika shule ya Baccalaureate nchini Ufaransa.Mwaka 1956.

Manu Dibango ni kiongozi wa bendi ya Makossa, yaelezwa kwamba kati ya mwaka 1949 -1954 Dibango alichukua masomo ya kupiga ala ya Piano na akanza kupiga muziki wa jazz. Alianza kupiga muziki rasmi mwaka 1954 akiwa na umri wa miaka 20.

Emmanuel Dibango  aligundulika kuwa ni mtu mwenye kipaji baada ya kuonekana alivyokuwa akipenda muziki, toka alipokuwa bado mdogo akiwa nyumbani na husan Kanisani ambako mama yake alikuwa kiongozi wa kwaya.  Manu alifahamika sana katika nchi  zote ambazo  zilitawaliwa na wafaransa huko Afrika ya Magharibi.

Ni mwanamuziki analiyejiwekea kumbukumbu kwa wapenzi wa muziki kwa wimbo wake uliotamba wa ‘Supa Kumba’ ambao alipipuliza  saxophone huku akiimba kwa kutumia sauti yake nzito iloyeleta mvuto wa aina yake miaka ya 1970.



Manu alikuwa mmoja kati ya waanzilishi muziki wa kidunia katika miaka 1970, na ameendelea kuhodhi hadhi ya kimataifa akiwa mwanamuziki wa kutegemewa katika muziki wa kiafrika miaka ya 1990.

Mwaka 1994, Boston Globe ilimpendekeza kuwa mwanamuziki bora kwa kibao chake cha ‘Wakafrika’ alipokea tuzo hizo akiwa na Nyota wa wanamuziki  toka Afrika na Ulaya akina, King Sunny Ade, Ladysmith Black Mambazo, Peter Gabriel, and Sinead O'Connor.

Ingawa Manu Dibango amekuwa akipingwa sana kwa kutumia sauti za kigeni za Waafrika,Wazungu na Wamerekani lakini alikuwa na msimamo madhubuti la kutetea alama yake katika muziki ‘Identity’

Muziki katika bendi yake ya Makossa ulipanda chati ambapo ulionekana ni wa kisasa zaidi kwa watu wa Cameroon huko Afrika  ya Magharibi mwaka 1973, baada ya kutoa album ya muziki wa Soul iitwayo Makossa.
 

Kama nilivyokujuza awali Dibango alipokuwa na umri wa miaka 15 akiwa na familia yake walikwenda nchini Ufaransa na yeye akaingia shule akisomea cheti cha Diploma.
Akiwa huko alisikia muziki wa Jazz wa ki-marekani na alitamka furaha yake kumsikia kwa mara ya kwanza radioni mwanamuziki Louis Armstrong.

Miaka ya 1940  Manu  Dibango ilielekeza nguvu zake katika upigaji wa chombo cha Saxophone akikabwaga chombo ‘kilichomtoa’ cha Piano ambacho ndicho alikuwa akikitumia.

Mwishoni mwa miaka ya 1950  Dibango alihamia nchini katika jiji la Brussels nchini Ubelgiji.
Akiwa huko miaka ya 1960 makubaliano ya kupatikana kwa Uhuru wa nchi ya Kongo yalikuwa yamefikiwa.

Manu Dibango pia alipiga muziki na wanamuziki wakongwe wa muziki katika Afrika waliokuwa wakiishi Ulaya akiwemo Joseph Kabasele ‘Grand Kale’ ambaye alikuwa mwimbaji nyota toka nchi ya  Kongo.
Baada ya Kongo kupata uhuru wake mwaka 1960 ikabadilishwa jina na kuwa Zaire.

Album yake  ya  Independence Cha-Cha, ikaja kuwa moto kwa wapenzi wa muziki Afrika na Ubelgiji hususan mji wa Brussels.

Mwaka 1961 Dibango alicheza na kurekodi nyimbo zaidi ya 100  nchini humo,  akishirikiana na Joseph Kabasele ‘Grand Kalle’ katika bendi ya African Jazz hadi ilipofika mwaka 1963, ambapo Dibango aliamua kurejea nyumbani kwao Cameroon baada ya kuiacha kwa miaka  12.

Hata hivyo mwaka 1965 alilazimika kwenda Paris nchini Ufaransa ambako wapenzi wa  muziki wake wa Soul katika jiji hilo walimuhitaji. Huko Paris,  akaanza  kupiga muziki wa kimataifa akitumia Saxophone yake.

Baada ya kupata mafanikio makubwa Dibango alitoa album nyingi za muziki wa kiafrika akichanganya na wa ule wa Jazz na Bleus.

Mwaka 1979 alijaribu kupiga muziki  wa  reggae, na alirekodi na baadhi ya wanamuziki wa kikundi cha The  Wailers huko Jamaica.  The Wailers ilikuwa ikimilikiwa na  hayati Bob Marley.

Manu Dibango mwaka 1984  alifanya sherehe kubwa ya kutimiza miaka 30 ya kupiga muziki, iliyowakutanisha wanamzuki wengine toka sehemu mbalimbali.

Mwanamuziki wa Ulaya  Sinead O'Connor na Peter Gabriel waliungana na wanamuziki nyota  toka Afrika Youssou N'Dour, King Sunny Ade, na Ladysmith Black Mambazo kurekodi na Manu  Dibango katika album yake ya mwaka 1994 iliyojulikana kama  ‘Wakafrika’

Nyimbo  zingine zilizompa umaarufu zilikuwa Supa Kumba aliyoitoa mwaka  1974 na Africadelic ya 1975.
Zingine ni pamoja na Gone Clear, Island, ya mwaka 1979, Ambassador, Island ya mwaka 1981, Waka Juju na Sonodisc, 1982, O Boso, ya mwaka 1971, Soma Loba, 1972, Soul Makossa, Atlantic, 1973, Super Kumba, 1974 na Africadelic ya  1975. Film scores L'herbe sauvage, Cote d'Ivoire, 1976,  Ceddo, Senegal  na  Le prix de la liberte, Cameroon za mwaka  1976.

Dibango alifytua vibao vingine vya  With Sly (Dunbar and Robbie Shakespeare) Gone Clear, Island ya mwaka  1979, With Dunbar and Shakespeare Ambassador, Island ya  1981, Waka Juju, Sonodisc iliyotoka mwaka 1982, Soft and Sweet ya mwaka 1983 na  Melodies Africans, Volumes 1 & 2, 1983. Manu Dibango  ni mwenye kipaji  ambacho kimefanya muziki wake kukubalika kimataifa kufuataia nimbo zake alizotunga na kuzipiga katika mataifa mbalimbali duniani. Mwaka 1984 aliachia nyimbo zingine za  Abele Dance, RCA  na mwaka uliofuatia 1985, Dibango akatoka na wimbo wa Electric Africa, Celluloid.
Kama vile hazitoshi Mzee mzima akaachia vibao vya  Afrijazzy, Soul Paris ya  mwaka 1986, Polysonic, iliyorekodiwa na  Bird Productions  mwaka  1990,   na  Live '91, FNAC Music, 1991. Mwaka 1994 akaja na album ya Wakafrika  ikiwa na nyimbo nyingi zikiwemo za   ‘ Soul Makossa,’ ‘Ca Va Chouia,’ na ‘Biko’. Mzee mzima Manu Dibango akamalizi kazi kwa kutengeneza wimbo wa  Giant mwaka  1994.


Mwisho.


No comments: